KATIBU
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Daniel Chongolo amewasili mkoani
Simiyu huku akipokewa na Viongozi wa CCM Wilaya na Mkoa na Viongozi wa
Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe.David Kafulila.
Ndugu
Chongolo amepokewa njia panda katika Kata ya Isanga wilaya ya Maswa
katika Jimbo la Maswa Magharibi, Simiyu leo Mei 31,2022 akitokea mkoani
Shinyanga
Ndugu
Daniel Chongolo ambae pia ni Mlezi wa Mkoa huo ameanza ziara ya kikazi
katika Mkoa wa Simiyu, ambapo pamoja na mambo mengine ni kuimarisha na
kuhimiza uhai wa chama kuanzia ngazi ya mashina.
Chongolo
ambaye ameambatana na Mjumbe wa Kamati Kuu na Katibu wa Halmashauri
Kuu ya CCM Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ngemela Lubinga pia
atazungumza na wanachama wa Chama hicho pamoja na kukagua miradi ya
maendeleo kama ilivyoahidiwa kwenye Ilani ya uchgauzi Mkuu mwaka
2020-2025.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...