Watumishi
wa Mamlaka ya Usafiri Ardhini (LATRA) leo Mei mosi wameungana na
watumishi wengine kusherehekea siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi)
ambayo Kitaifa imefanyika Dodoma na Dar es Salaam yakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla katika Uwanja wa Uhuru uliopo Temeke jini Dar es Salaam.
Watumishi
watatu kutoka LATRA ambao ni Bw. Philipo Ngongi, Bi. Habiba Chambali
pamoja na Bw. Thomas Matope wametunukiwa utumishi bora na kupongezwa
na Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam Amos Makalla.
Maadhimisho
ya mwaka huu yamebebwa na Kaulimbiu isemayo "Mishahara na Maslahi Bora
kwa Wafanyakazi Ndio Kilio Chetu. Kazi Iendelee".
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla akimpongeza Mfanyakazi wa
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) Philipo Ngongi mara baada
ya kutangazwa kuwa mfanyakazi Bora kwenye Maadhimisho ya Siku ya
Wafanyakazi Duniani mwaka 2022 yaliyofanyika kimkoa katika Uwanja wa
Uhuru Jijini Dar es Salaam.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wakiwa kwenye
maandamano kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka 2022
yaliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam
Wafanyakazi
Bora wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wa kwanza kushoto
ni Thomas Matope, kati ni Habisa Chambali na kulia ni Philipo Ngongi
wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada kutangazwa kuwa wafanyakazi
Bora kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka 2022
yaliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi
Bora wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wakiwa kwenye
picha ya pamoja na viongozi pamoja na wafanyakazi wenzao wa LATRA mara
baada ya kutangazwa kuwa wafanyakazi Bora kwenye Maadhimisho ya Siku ya
Wafanyakazi Duniani ambayo yamefanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar
es Salaam.
Wafanyakazi
wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wakiwa Uwanja wa Uhuru
wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka 2022 yenye Kaulimbiu isemayo "Mishahara na Maslahi Bora kwa Wafanyakazi Ndio Kilio Chetu. Kazi Iendelee"
Wafanyakazi
wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wakiwa kwenye picha ya
pamoja mara baada ya kumalizika kwa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi
Duniani mwaka 2022 yaliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es
Salaam.
Gari
la Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) likipita kwenye
maandamano ya Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka 2022
yenye Kaulimbiu isemayo "Mishahara na Maslahi Bora kwa Wafanyakazi Ndio
Kilio Chetu. Kazi Iendelee" yaliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini
Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...