Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze
MKUU
wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallah ameeleza miradi 25 yenye thamani
ya Bilioni 47.2 inapitiwa na Mwenge wa Uhuru kati ya miradi hiyo ni
pamoja na kuweka jiwe la msingi mradi wa kipekee wa Ufugaji Afrika
Mashariki na Ukanda wa Sahara .
Akipokea
mbio za Mwenge wa Uhuru ukitokea wilaya ya Kibaha, huko Ruvu Darajani
alieleza wilaya hiyo ina Halmashauri mbili ambapo Halmashauri ya
Chalinze itatembelewa miradi 14 iliyogharimu milioni 937.8 na Bagamoyo
miradi 11 yenye thamani ya Bilioni 46.3.
Aidha
alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia Bilioni 1.6 fedha za
Uviko Chalinze na kujenga madarasa na miradi 66 ya shule za Sekondari .
Mkuu
huyo wa wilaya alieleza kwamba, kwa Halmashauri ya Bagamoyo imepokea
Bilioni 1.02 na kujenga shule shikizi 14 na Sekondari 37.
"Tunamuahidi
Rais Samia kuwa hatutamuangusha ,katuteua kumsaidia kazi na hapa kwetu
Chalinze na Bagamoyo tunapiga kazi ili kuleta maendeleo"alisema Zainab.
Zainab
alifafanua, wilaya hiyo inategemea zaidi chanzo Cha mapato ya ndani Cha
kokoto na mawe ambayo yanapelekwa jijini Dar es Salaam na maeneo
jirani.
"Asilimia 60 ya
mapato ya ndani yanatokana kwenye kokoto na mawe, ndio maana sisi miradi
yetu ipo vizuri kwakuwa tunatumia malighafi inayotoka kwetu wenyewe
"alisisitiza Zainab.
Vilevile
akizungumzia suala la sensa ya watu na makazi alieleza, Zoezi la anwani
na makazi wameshalitekeleza kwa asilimia 100 Hadi Sasa.
Mbunge
Wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema ushauri, mapungufu
wanayopatiwa watayafanyia kazi ili baadae miradi iwe Bora kwa maslahi
mapana ya wananchi wa Chalinze.
Kiongozi
wa mbio za mwenge Kitaifa Sahir Geraruma alihimiza usimamizi makini wa
miradi kwani Serikali inatumia fedha nyingi hivyo inatarajia matokeo
chanya yenye tija kwa Watanzania.
Miradi
iliyopitiwa Chalinze ni pamoja na kuona shughuli za usafirishaji abiria
-pikipiki ambao umegharimu milioni 41.8 kati ya fedha hiyo mil.32.6 Ni
mkopo wa asilimia 4 ya vijana kutoka Halmashauri na milioni 9.2 Ni fedha
ya wanakikundi na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la wodi ya
mama na mtoto pamoja na upasuaji kwa fedha ya tozo.
Pia kuzindua mradi wa ukarabati wa barabara Pingo, kufungua vyumba viwili vya Madarasa na ugawaji wa vifaa vya ujenzi vinavyotokana na asilimia 5 ya mchango ya mwenge, kufungua kituo cha afya Sekondari Imperial, mradi wa kisima Kibiki na kuzindua ujenzi wa madarasa manne ya uviko19
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...