MCHEZAJI wa Pooltable anayeshikilia kiwango cha namba moja Tanzania, Abdallah Hussein(Dullah) leo mapema ameondoka kuelekea Uganda kwenye Mashindano ya wazi "PAU Pool Grand Open" yaliyoandaliwa na Chama cha Pool nchini Uganda(PAU).

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii May 28 - 29, 2020 katika Ukumbi wa SEETA Kampala Uganda kwa kushilikisha Wachezaji nguli(Maarufu) Afrika ambao tayari wameshathibitisha kushiriki.

Wachezaji waliothibitisha kushiriki ni kutoka, Afrika Kusini, Zambia, Kenya, Tanzania na wenyeji Uganda.

Abdallah Hussein (Dullah) ametamba kwenda kufanya vizuri kwenye mashindano hayo baada kushiriki mashindano ya Afrika Mashariki hivi karibuni yaliyofanyika Nchini Kenya nakupata uzoefu wa kutosha.

Alisema Dullah, 'Nina ndoto za mbali sana za kuitangaza Nchi yangu ya Tanzania kupitia mchezo wangu wa Pool, naomba sana Wafadhili wangu, ndugu zangu, marafiki zangu na Watanzania kwa ujumla mniombee' alimaza Dullah huku akiingia kwenye Bus likielekea Kampala Uganda.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...