NA MWANDISHI WETU, TANGA
MFUKO
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika
maonesho ya bishara na utalii kwa kutoa elimu kwa wanachama kupitia
maonesho yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako jijini Tanga.
PSSSF
inashiriki katika maonesho haya pamoja na kutoa elimu kwa wanachama na
wananchi wanaotembelea banda hilo, pia wanachama wanapatiwa huduma
mbalimbali za kiofisi ikiwemo, kuangalia taarifa za michango ya
wanachama, taarifa za malipo ya pensheni, uhakiki wa wanachama na kutoa
ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya uanachama, alisema Bi. Rehema
Mkamba, Afisa Mkuu wa Uhusiano, PSSSF
Alisema
ni fursa nzuri kwa Mfuko kukutana na wanachama wake lakini wananchi pia
ambao watafika kwenye maonesho hayo maarufu kama Tanga Trade Fair
ambayo yatadumu kwa siku 10 kuanzia Mei 28 hadi Juni 6, 2022.

Wananchi na wanachma waliofika kwenye banda la PSSSF weakijisajili kwenye kitabu cha wageni baada ya kuhudumiwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...