Na.Vero Ignatus,Arusha

Suala la Uhuru kwa vyombo vya habari bado ni suala mtambuka kwani waandishi wengi wa habari duniani wamekuwa wakipitia  changamoto nyingi za Unyanyasaji wakijinsia haswa waandishi wa kike jambo ambalo  limetapakaa zaidi haswa kwenye  unyanyasaji wa kingono

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAMWA Dkt.Rose Reuben katika Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani, linaloendelea Jijini Arusha kwamba waandishi wengi Kumekuwa na changamoto nyingi  wamekuwa wakipitia waandishi wa habari Ulimwenguni ikiwemo maslahi duni ya Waandishi ambayo hayapigiwi kelele hadi sasa

"Tunaamini kwamba Vyombo vya habari tunao uwezo wa kumaliza Ukatili wa Kijinsia kwa kuandika habari zinazolaani na Kupinga unyanyasaji huo "alisema Dkt.Rose

Dkt Rose alisema kuwa pamoja na Changamoto ya mabadiliko ya kiteknolojia ,uandishi wa habari unabakia Kama uandishi kwasababu ni taaluma,hivyo wanahabari wakikubaliana kwa pamoja kwenda kuandika kwa mabadiliko mambo mengi yatabadikika vilevile,wao wenyewe tutabadikika,na taaluma ya habari  itaheshimika 

Kwa Upande wake Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya habari Nape Nauye Amesema kuwa wahabari wanao Wajibu wa kukabiliana na changamoto zilizopo na kulisaidia Bara la Afrika na kuhakikisha  rasilimali zilizopo  zigeuke kuwa baraka na siyo mafarajano,ili lifaidike na wananchi wao wajivunie kuwa kwenye Bara lao.

"Ukilingamisha rasilimali zilizopo Afrika na sisi tulivyo hatupaswi kuwa Kama tulivyo Sasa ifike wakati waandishi wa habari mtutumie kalamu zenu vyema kuisaidia Jamii kuziona fursa zilizopo"alisema Nape

Amesema kutokana na mada mbalimbali zitakazojadiliwa katika kongamano hilo la Uhuru wa Vyombo vya habari, watumie msingi katika kuendeleza,shughuli za wanahabari katika kupata Elimu mbalimbali ikiwemo wa sheria,sheria ya kupata taarifa pamoja na kanuni zake 2016,itasaidie kupata uzoefu utakaosaidia mchakato wa mapiitio ya sheria hiyo

Amewataka  washiriki kujadiki kwa kina changamoto zinazowakabili sekta ya habari Barani Afrika,ulinzi na Usalama wa waandishi wa habari, ili waone ni namna gani wanaweza kuzitatua katika nyakati hizi za ukuaji wa teknolojia za habari 

Kwa Upande wa Balozi wa  EU nchini  Tanzania Manfredo Fanti amesema kuwa Kuhakikisha kuwa Kuna uhuru na Usalama ka waandishi wa habari ni changamoto ya dunia ,kwani zaidi ya mashambulizi ya kidigitali 439 yamefanywa kwa  waandishi wa habari, yameleta changamoto na wengine kuwashambuliwa kwa maneno na kuweka hatarini.

Akitolea mfano wa vita inayoendelea nchini Ukren amese kuwa habari za uongo zinatumika na kupunguza kutambulika kwa tasnia ya uwaandishi wa habari , hivyo Umoja wa Ulaya unaandaa sheria ya kulinda uhuru wa vyombo vya habarinkama vile ambavyo mwaka 2021,ambapo umoja huo ulileta sheria ya kuilinda waandishi wahabari 

Amezitaka Taasisi mbalimbali kuwasaidia waandishi wa habari kuwasaidia waandishi pale akaunti zao zinapoingiwa na uhalifu wa kimtandao ,pamoja na changamoto za Kijiditi katika nchi za Ulaya ambapo umoja huo unatekeleza mikakati mbali katika hilo haswa uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza na kulinda haki za binadamu

Hadi Sasa tumeweza kuwasaidia waandishi 550  Ulimwengu  kote kutokana na program mbalimbali tulizoziweka"

Mkuu wa Mawasiliano Win Mussabayana kutoka  Umoja wa AFRIKA  amesisitiza kuwa ,umoja huo unamamlaka katika nchi 55 Barani katika kuhakikisha Kuna Maendeleo na utengamano Barani Afrika na kuhakikisha ipo katika ngazi za dunia

Amesema Afrika inatakiwa kuondokana na dhana ya zamani inayoonejana kuwa afarika ni Bara la magonjwa ,rushwa na umasikini hivyo wanahabari
wanayo nafasi kwaajili ya kusimamia hilo na kubadilisha dhana hiyo  kwenye agenda ifikapo 2063 kuelezwa mtazamo mpya wa AFRIKA

 Mkurugenzi wa UNESCO Kanda  Afrika Mashariki Prof.Hubert Gjzen amesema kuwa ni Furaha yake kubwa kujumuika na wanahabari siku ya leo katika siku ya uhuru wa vyombo vya habari na kusema.kuwa siku hii ni muhimu kwa Bara lote la Afrika

Amesema.Tanzania imeondoa vikwazo vya vyombo vya habari 4 na kurahisisha upatikanaji wa habari na kulinda uhuru na Hali ya msingi Kama ilivyoainishwa kwenye Maendeleo endelevu no 16
1945 UNESCO imekuwa mpiganaji  mkubwa wa Haki za binadamu ambapo 1991 ulianzishwa mapambano Dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari Windsock Namibia  huru wa vyombo ambapo Sasa umri wa miaka 30

"Nimesikitishwa Sana wakati wa kanga la COVID 19 habari nyingi zilikuwa za uongo na uzushi haswa kwenye majukwaa ya kidigiti na tunathubutu kusema kuwa tasnia imeingiliwa hivyo tunahitaji kusisitiza jukumu la vyombo vya habari ili kulinda faragha za watu" alisema

Kwa mwaka 2021 washiriki wa uhuru wa vyombo vya habari walipitisha azimiao la windowck kwmaba Tunatakiwa kulinda Usalama wa waandishi wa habari mahali pa kazi nankuzingatia changamoto mpya zinazoletwa na teknolojia.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri nchini Tanzania Deodatus  Balile amesema kwa Mara ya kwanza, shughuli hiyo ya uhuru wa vyombo vya habari kutoka nchi 54 Barani Afrika  na wageni wasiopungua 100 ambapo siku ya kwanza zaidi ya 280.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe.  Nape Nnauye akizungumza wakati akifungua maonesho mbalimbali kuelekea maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani yatakayofanyika Mei 3,2022 jijini Arusha.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho mbalimbali kuelekea maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani yatakayofanyika Mei 3,2022 jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Deodatus Balile, akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho mbalimbali kuelekea maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani yatakayofanyika Mei 3,2022 jijini Arusha.

Mkurugenzi wa Mawasilianon wa Tume ya Muungano wa Umoja wa Afrika, Musabayana Wynne Zvinaiye akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho mbalimbali kuelekea maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani yatakayofanyika Mei 3,2022 jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...