Na.Khadija Seif, Michuzi TV

WAFANYABIASHARA hususani wanaofanya Huduma katika sherehe wametakiwa kujiunga na Benki Ili waweze kukopesheka kusaidia kukuza Biashara zao pamoja na kutunza akiba.

Akizungumza jijini Dar es salaam wakati akifungua Maonyesho ya Biashara ya wahudumu katika Sherehe (Adorable wedding trade fair) Msimu wa 5, Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo Ibrahim Mwangalaba amesema ni Muhimu Wafanyabiashara kuweka akiba zao na kufunga akaunti za kibenki Ili kujiwekea umakini wa biashara zao pale mteja anapotaka kutuma muamala kwa njia za kibenki kuliko kutoa maelezo ya kutumiwa Fedha Kwa njia ya Mitandao ya simu.

Hata hivyo Mwangalaba ametoa wito Kwa Wafanyabiashara hao kuendelea kukuza Biashara zao na kutengeneza Mawasiliano wao Kwa wao kwani kufanya hivyo ni kujenga Mahusiano mazuri kwenye fani hizo na kuboresha kazi zao .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa My wedding solution ambae pia ni Mratibu wa Maonyesho hayo Anna Rema amesema Maonyesho hayo yanaendelea kukuwa zaidi Huku lengo lake likiwa ni kuandaa Maonyesho ya Afrika Mashariki .

Rema amesema Maonyesho hayo yatachukua siku 3 na wanatarajia Mgeni rasmi wa kufunga Maonyesho hayo Mei 15 ni Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mohamed Mchengerwa.

picha ya pamoja kati ya washiriki wa Maonyesho ya Biashara ya wahudumu katika Sherehe na Wafanyabiashara wengine pamoja na Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo nchini Ibrahim Mwangalaba wakati akizundua rasmi Msimu wa 5 wa Maonyesho hayo katika ukumbi wa Mlimani city Jijini Dar es salaam.
Emmal cakes ni Miongoni mwa Banda aliliotembelea Mgeni rasmi ambae ni Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo Ibrahim Mwangalaba na kueleza jinsi gani utengenezaji wao wa keki ni wakibunifu zaidi kutokana na kutengeneza keki za Maumbo mfano wa Nyumba za kuishi za kifahari.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...