Picha ya Pamoja.

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Utangamano na Frankafoni, Mheshimiwa Didier Mazenga katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara Mtumba Dodoma.

Mazungumzo yao yalihusu kuimarisha ushirikiano wa kindungu na wa kihistoria baina ya nchi hizi mbili uliodumu kwa miaka miaka mingi tangu nchi hizi zipate uhuru.

Mambo mengine waliyojadiliana ni kuhusu kubadilishana uzoefu wa kuiongoza Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) kwa kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inatarajia kuchukua uenyekiti wa Jumuiya hiyo ifikapo mwezi Agosti mwaka huu, Jumuiya ambayo Dkt. Stergomena amewahi kuisimamia kwa takribani miaka minane akiwa Katibu Mtendaji tangu mwaka 2013 na kumaliza muda wake rasmi mwezi Agosti mwaka jana.

Aidha, DR Congo kama mwanachama wa Jumuiya hiyo amekuwa wakishirikiana na Tanzania katika maeneo mengi yakiwemo ya ushirikiano kupitia nyanja za ulinzi na usalama. Kwa maana hiyo mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha ushirikiano zaidi kupitia sekta hii.

Kwa kuwa DR Congo ni mwanachama mpya katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), mawaziri hao pia, wamejadiliana ni kwa namna gani wanaweza kushirikiana na hatimaye kuweza kuleta maendeleo na Ustawi wa nchi hizi mbili.

Utangamano wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unachagizwa zaidi na utatu, kwa kuwa wote ni wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi wanachama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...