Mtendaji Mkuu wa BRELA Godfrey Nyaisa akizungumza katika semina ya siku tatu iliyowakutanisha Maafisa Biashara kutoka katika Mikoa minne ambayo ni Dar es salaam, Lindi, Mtwara na Pwani.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Biashara hao

Na Khadija Kalili
MTENDAJI Mkuu wa Wakala wa Usalini wa Biashara na Leseni (BRELA) Godfrey Nyaisa amewataka maafisa biashara kutoka nje ya Ofisi zao ili kwenda kuzitambua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi na kuzipatia utatuzi.

Akizungumza leo katika semina ya siku tatu iliyowakutanisha Maafisa Biashara kutoka katika Mikoa minne ambayo ni Dar es salaam, Lindi, Mtwara na Pwani.

Katika semina hiyo Maafisa Biashara hao pia wametakiwa kutumia fursa za kukutana na wafanyabiashara katika Mikoa yako pamoja na kuangalia namna watakavyoweza kubuni fursa mpya za biashara ili kuweza kukuza kipato na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge amewaeleza Maafisa Biashara hao kuwa kuwa anawaagiza wakajifunze kusoma bila kuchoka na kuhakikisha wanazingatia mafunzo hayo na pindi watakaporudi katika Mikoa yao waweze kuonyesha matokeo chanya ya mafunzo waliyoyapata.

"Hivi Sasa mafunzo kama haya ni muhimu kwenu ili kufanya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassani katika kuvutia wawekezaji katika nyanja ya biashara nchini hii hatima iko mikononi mweni kwani jukumu la kukuza uchumi wa nchi kunaanzia ngazi ya Mkoa." Amesema Kunenge.

"Fursa hii ni nzuri hivyo ni matarajio makubwa ya serikali kwenu Maafisa Biashara ingieni mtaani mkasikilize kero za wafanyabiashara" Amesema Kunenge.

RC Kunenge ameongeza kwa kusema kuwa lazima Maafisa Biashara wayajue huduma bora ambazo wanapaswa kuzitoa kwa wananchi na zipi hawapwi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...