Na Pamela Mollel,Arusha 
Mkuu wa wilaya ya Arusha,Said Mtanda amewafunda wastaafu watarajiwa mkoani hapa,kufanya matumizi sahihi ya fedha za mafao yao pindi wanapolipwa na kuacha kujiingiza kwenye starehe na kununua magari mabovu badala yake wajikite katika kuanzisha miradi vijijini au kuwekeza hisa kwenye mabenki

Pia aliwashauri kurudi kijijini kuanzisha miradi ya kisasa ya kilimo ,ufugaji na viwanda vidogo hatua itakayosaidia kunufaika na mafao yao kuliko kukimbilia kununua magari mabovu ya biashara au kujenga nyumba ya kupangisha jambo litakalopelekea kutapeliwa na kujikuta wakifilisika.

Kauli hiyo ameito wakati akifungua semina ya siku mbili ya wastaafu na wanachama wa mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF , wapatao 300,semina iliyolenga kuwajenga kisaikolojia, ambapo pia aliwashauri kuhakikisha wanawekeza kwa kununua hisa kwenye mabenki na kujiweka salama na fedha zao.

Alisema kumekuwepo na tabia inayojitokeza kwa wastaafu pindi wanapolipwa mafao yao ambapo baadhi yao hujiingiza kwenye starehe na kuona vibinti vidogo ambao huwaibia fedha zao na muda mfupi huishiwa na kubaki wakihangaika hapa mjini.

Aliwataka wastaafu hao kutoogopa maisha mapya bali wazingatie kazi na matumizi sahihi ya fedha watakazolipwa kwa kwenda kuanzisha miradi vijijini au kuwekeza kwenye hisa kwenye benki

" Epukeni starehe za kuoa mabinti wadogo watakaowaponza na kufilisika au kwenda kununua magari mabovu ya biashara"alisema

Alisisitiza kuwa dhana ya kukimbilia kununua Magari ya biashara hususani Coaster ni ushauri mbovu kwa sababu wengi wao wanashauriwa bila kuwa na utaalamu wa biashara hiyo ,epukeni uwekezaji usio sahihi.

Awali meneja usimamizi wa mafao kutoka NSSF Taifa,James Galusoigo alisema semina hiyo inalenga kuwaanda wastaafu watarajiwa wanaokaribia kustaafu wenye umri kati ya miaka 55 hadi 60 ili kuhakiki kumbukumbu zao mapema baada ya ujio wa mfumo wa NIDA ili kuepuka kucheleweshewa mafao yao.

Alisema kuwa NSSF imefanya mabadiliko makubwa katika mfumo wake wa malipo ambapo mstaafu aliyekamilisha vema kumbukumbu zake atapokea mafao yake ndani ya mwezi mmoja baada ya kustaafu.

Kwa upande wake Josephat Komba meneja wa NSSF Mkoa wa Arusha,alisema semina hiyo ni fursa nzuri kwa wastaafu katika kuwajengea uwezo juu ya matumizi sahihi ya mafao yao .

Alisema washiriki wa semina hiyo ni wanachama wa mfuko wa NSSF kutoka kampuni na taasisi mbalimbali mkoa wa Arusha ambao wanatarajiwa kustaafu hivi karibuni 

Alitoa wito kwa waajiri kuhakikisha wanawasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati ili kuepuka ucheleweshaji wa malipo ya mafao pindi wanapostaafu.

Baadhi ya washiriki wa semina hiyo Issa Mohamed au Onyango Kanindo msanii mchekeshaji,Steven Mwilolezi na Justine Lyela walisema semina hiyo imekuja wakati mwafaka kwani itasaidia sana kuwaanda wastaafu kisaikolojia ambao wengi wao wamekuwa wakitapeliwa mafao yao na kujikuta wakiadhilika na kuwa ombaomba.
Mkuu wa wilaya ya Arusha Said Mtanda akizungumza na wastaafu watarajiwa kuhusu fedha za mafao pindi wanapolipwa kufanya matumizi sahihi ya fedha hizo
Mchekeshaji maarufu hapa nchini Onyango Kanindo akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa NSSF Mkoa wa Arusha Josephat Komba akizungumza katika semina hiyo
Mstaafu mtarajiwa Steven Mwilolezi akizungumza na waandishi wa habari



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...