Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Shirikisho la Soka duniani (FIFA) limeifungia Klabu ya Geita Gold FC inayoshiriki Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kusajili Wachezaji hadi itakapomlipa Aliyekuwa Kocha wake Mkuu, Etienne Ndayiragije anayedaiwa kudai malipo yake ya fidia ya kuvunjiwa mkataba na malipo mengine wakati akiifundisha timu hiyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) imeeleza kuwa kwa mujibu wa taratibu za FIFA endapo Geita Gold FC itakuwa haijamlipa Etienne suala hilo litawasilishwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya FIFA kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu.

TFF imeendelea kuzikumbusha Klabu za Soka nchini kuheshimu mikataba ambayo inaingia na Wachezaji na Makocha kutokana na vigezo vya kupata Leseni ikiwa ni utekelezaji wa Kanuni ya Leseni za Klabu (Clubs Licensing Regulations).

Kocha Etienne Ndayiragije aliwahi kuifundisha Klabu ya Geita Gold FC ya Geita ambayo inashiriki Ligi Kuu Soka Tanzania Bara msimu huu wa 2021-2022 kabla ya kufutwa kazi kutokana na matokeo yasiyoridhisha ambapo nafasi yake alichukua Kocha Msaidizi, Fred Felix Minziro.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...