NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Morogoro

MAAFISA Kazi nchini wameaswa kuwa waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Jamal Katundu amesema mjini Morogoro Juni 18, 2022 wakati akifungua kikao kazi baina ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Maafisa Kazi nchini chenye lengo la kuwajengea uelewa wa maboresho ya sheria ya fidia kwa wafanyakazi.

“Nichukue nafasi hii kuwakumbusha kwamba uadilifu ni jambo la msingi sana katika kazi zinazofanywa katika Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake ninyi mkiwemo,hakikisheni taarifa za ukaguzi zinakuwa za  kweli na sahihi msiingie kwenye vishawishi” alisema

Alisema Maafisa Kazi nchini ni mabalozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, na wanapaswa kuwa na uadilifu wa hali ya juu, WCF ipo Ofisi ya Waziri Mkuu hivyo wanapaswa kutekeleza majukumu yao ili kuweka heshima ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Aidha Kamishna Mkuu Idara ya Kazi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Suzan Mgangwa amesema idara yake na WCF zimeazimia kufanya kazi kwa pamoja ili kuendelea kulinda mfanyakazi nchini wanapopata majanga wakati wakitekeleza majukumu yao.

Akizungumza mwanzoni mwa kikao hicho, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini WCF, Bi. Rifai Mkumba alibainisha kuwa katika muktadha wa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Bodi imeendelea kusisitiza umuhimu wa Mfuko kuendelea kutoa elimu kwa wadau ikiwa ni pamoja na taasisi mbalimbali hususan za serikali wakiwemo Maafisa Kazi ili kukuza uelewa kuhusu masuala ya fidia ikiwemo huduma mpya kama zilivyoboreshwa na serikali.

Naye  Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma alisema lengo la kikao kazi hicho ni kujengeana uwezo ili kuwa na uelewa wa pamoja.

“Mabadiliko ya kisera, mabadiliko ya kisheria na kanuni na mabadiliko ya kiutendaji yaliyotokea kwenye mifumo ambayo inatumika kwenye utekelezaji wa shughuli za Mfuko kwa hiyo kikao hicho kitasaidia kuona maendeleo ya mabadiliko hayo.” Alisema Dkt. Mduma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Jamal Katundu, akizungumza na Maafisa Kazi nchini, kwenye kikao kazi baina ya Maafisa hao na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyamkazi (WCF) mjini Morogoro Juni 18, 2022.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Jamal Katundu
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini WCF, Bi. Rifai Mkamba akizungumza kwenye kikao hicho.
Baadhi ya Makamishina na Maafisa Kazi nchini wakiwa kwenye kikao hicho
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma, akizungumza na Maafisa hao.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma, akizungumza na Maafisa hao.
Profesa Katundu akipongezwa na Dkt. Mduma (kushoto) na Bi. Suzan baada ya kutoa hotuba yake ya ufunguzi.
Profesa Katundu (kulia) akifurahia jambo na Dkt. Mduma.
Viongozi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ambao ndio waliotoa elimu kuhusu uelewa wa maboresho hayo ya sheria.
Viongozi wa WCF kutoka kushoto, Dkt. Abdulsalaam Omar (Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini), Bw. Abraham Siyovelwa (Mkuu wa Kitengo cha Sheria(, Bw. Anselim Peter (Mkurugenzi wa Uendeshaji) na Bw. Bezil Ewala, Mkurugenzi wa Fedha, Mipango  na Uwekezaji wakibadilishana mawazo muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao hicho.
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Elimu kwa Umma WCF, Bi. Laura Kunenge akieleza utaratibu wa namna kikao kazi hicho kitakavyoendeshwa.
Kamishna Msaidizi wa Kazi, Bi. Rehema Moyo akinakili masuala muhimu yahusuyo maboresho ya sheria ya fidia kwa wafanyakazi
Baadhi ya washiriki
Baadhi ya washiriki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...