Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU
wa Mkoa wa Pwani, alhaj Abubakar Kunenge ametoa Rai kwa Maafisa
Biashara wa Mikoa ya Pwani, Dar es salaam, Lindi na Mtwara kuhakikisha
Jitihada za Serikali awamu ya sita za Kuvutia Wawekezaji
zinafikiwa,ikiwa Ni Pamoja na kuchangamka Kuwa wabunifu katika kubuni
vyanzo vipya .
" Rais
Samia Suluhu anavutia Wawekezaji na ameshasema nini kifanyike jinsi
gani hayo yanatekelezeka Maafisa Biashara mnapaswa kufanya, Vinara wa
Utekelezaji ni ninyi Maafisa Biashara tuone Uwepo wenu (Visibility).
Lazima muelewe matarajio ya Nchi ili muyatimize.
Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea Uwezo Maafisa Biashara wa Mikoa ya Pwani, Dar es salaam, Mtwara na Lindi.
Amewaeleza
kuwa Serikali imeamua kuanzisha Idara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji
Ofisi ya Rais TAMISEMI ili kuongeza ufanisi wa Sekta hiyo.
Amewataka kuhakikisha wanatoa huduma Bora kwa Wawekezaji na Wafanyabiashara.
"Lazima
tutoe huduma bora, lazima tujue wateja wetu ni Wafanyabiashara, huduma
bora inabadilika mara kwa mara kwa Wafanyabiashara" Ameeleza Kunenge.
Amewaeleza
kuwa Tanzania tupo eneo la Kimkakati Strategic position na kila Afisa
Biashara anatakiwa kujua Fursa za Uwekezaji zilizopo kwenye Eneo lake.
Amewataka
kusoma na kutumia Takwimu za Taasisi mbalimbali katika Kushauri na
Kufanya Maamuzi "Wawekezaji wanapokuja manawapa Takwimu gani? Amehoji
Kunenge-
"Wajibu wenu
kuhakikisha Spidi ya Teknolojia mnakwenda nayo mkishindwa mtakuwa
hamfai Maafisa Biashara mnatakiwa msome kila kitu" amesitiza Kunenge
Ameeleza
kuwa utafiti unaonesha Maafisa Biashara wanatumika zaidi kama
wakusanya Mapato badala ya kuwa wasaidizi na washauri wa
Wafanyabiashara na Wawekezaji.
Amewataka baada ya mafunzo hayo kubadilisha fikra na mitazamo yao na kuwa watoa huduma na msaada kwa Wafanyabiashara.
Nae
Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa Amewataka Maafisa
Biashara hao kutokuwa maafisa Biashara wa Ofisini badala yake kuwasadia
na Kushauri Wafanyabiashara.
Hata
hivyo ,amekemea tabia ya baadhi ya Maafisa Biashara kufoji Leseni za
Biashara Daraja B na kuwaeleza kuwa sasa wameandaa mfumo ambapo leseni
zote zitatolewa kwa njia ya mtandao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...