Na Mwamvua Mwinyi, Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alhaj Abubakar Kunenge ,amekagua Maendeleo ya Mradi Sukari (Kilimo cha Muwa na Kiwanda cha Sukari CAKaha Lake Agro Investment Ltd) kilichopo Utete Wilayani Rufiji ,unaotarajia kuzalisha Tani100,000 za sukari kuondoa Nakisi ya sukari kwa nchi na nyingine kuuza nje ya Nchi.

Akizungumza akiwa Eneo la Mradi Kunenge ameeleza wawekezaji hao wapo kwenye matayarisho ya Uwekezaji na kuwa Eneo hilo lina ukubwa wa Hekta 15 ambalo lote litakuwa kwa ajili ya Kilimo cha miwa .

Amesema wawekezaji hao tayari wamejenga njia ya umeme iliyogharimu zaidi ya Shilingi Milioni 100 na Barabara inajengwa, Matarajio ya Mkoa na Serikali kwa Mradi huo ni kupata Kodi,Ajira ya kutosha zaidi ya watu 18,000 ,Wananchi watapata utaalamu kwa sababu wawekezaji hawa watatumia teknolojia ya kisasa ambayo vijana wetu watajifunza na Mchango wa wawekezaji hao kwa Jamii (CSR).

" Tumekubaliana kwa sababu mradi huu ni Mkubwa paanze kupimwa na kupangwa tupate mji unaojitegemea,tupate Maduka sehemu za huduma za Jamii Masoko na makazi "

“kutakuwa na wakulima wengine wa nje Outgrowers ambapo mwekezaji yupo tayari kuwapa msaada wa kitaalamu ili wachangie kuuza miwa kiwandani”Kunenge alisema.

Naye Mwakilishi wa Kampuni ya Lake Agro Investment Abubakar Nassor amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa Mazingira mazuri ya Uwekezaji na Ushirikiano wanaoupata kutoka Uongozi wa Mkoa.

Ametoa Wito kwa Wananchi kuchangamkia Fursa hiyo kwa Kushiriki kwenye uchumi huu kwa kulima Miwa kwa wale wakulima wa Nje (Out growers) Wafanyabiashara kuleta huduma na kujipatia kipato.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...