WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa akipata malezo kutoka kwa Mkuu wa Shule ya Seondari Mandarawe, Mwalimu Ladia Juma (kushoto) kuhusu ujenzi wa Shule hiyo wilyani Ruangwa, Juni 3, 2022.
 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wazazi na walezi washirikiane na walimu katika kuwalinda watoto wa kike na wa kiume ili waweze kutimiza ndoto zao kielimu.

Pia, Waziri Mkuu amewataka watoto hao wasikubali kudanganywa na watu wasiopenda maendeleo yao na badala yake wasome kwa bidii na wahakikishe malengo yao kielimu yanatimia.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 3, 2022) alipozungumza na wanafunzi, wazazi na walimu katika shule ya Sekondari Mandarawe wilayani Ruangwa akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo.

“Kwa sasa kielimu wilaya yetu imepiga hatua kubwa, wanafunzi someni kwa bidii na Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kwamba inawawezesha kutimiza malengo mliyojiwekea.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema Kata zote za Wilaya hiyo zina shule za sekondari na tayari wameanza ujenzi wa mabweni, lengo likiwa ni kuwapunguzia wanafunzi adha ya umbali mrefu kwenda shuleni.

“Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa kila mtoto wa Kitanzania aliyefikia umri wa kwenda shule apelekwe shule na elimumsingi inatolewa bila ada nchini kote.”

“Kwenye suala la elimu tumejipanga vizuri na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametuunga mkono kwa kutupa sh. milioni 700 za ujenzi wa shule ya sekondari wasichana ya mchepuo wa Sayansi.”

Pia, Waziri Mkuu amekagua ujenzi wa Kituo cha Afya cha Namichiga na ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi wasimamie vizuri mradi huo na wahakikishe fedha zinatumika vizuri.

Mbali na kukagua ujenzi wa kituo hicho, pia Waziri Mkuu alikagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo vya Afya cha Kata ya Narungombe pamoja na maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya cha Nangurugai.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Majaliwa amewasisitiza wananchi wahakikishe wanatunza mazingira na kuacha kukata miti hovyo. “Tutunze mazingira na tusilime katika vyanzo vya maji.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...