Na. A/INSP FRANK LUKWARO
Kutokana na kuongezeka kwa matukio na vitendo vya Ukatili wa Kijinsia na Unyanyasaji dhidi ya Watoto, Jeshi la Polisi nchini lipo katika hatua za mwisho kulifanya somo la Ukatili wa Kijinsia na Ukatili dhidi ya watoto kuwa somo linalojitegemea katika vyuo vyake ili kukabiliana na vitendo hivyo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto, Naibu Kamishna wa Polisi Maria Nzuki wakati wa ufunguzi wa kikao cha kuhuisha mitaala ya Jeshi la Polisi kinachofanyika Shule ya Polisi Tanzania Zamani CCP na kuwashirikisha Wakuu wote wa Vyuo vya Polisi na Kamisheni zote za Polisi.

Kwa upande wao Baadhi ya Wakuu wa Vyuo vya Polisi Wamesema kwa sasa masuala ya Ukatili wa Kijinsia na Unyanyasaji yanafundishwa kwa kiwango kidogo hivyo itakapokuwa somo linalijitegemea itaongeza weledi Zaidi kwa Askari katika kukabiliana na vitendo hivyo.

Kwa Upande wake Mwakilishi kutoka Shirika la UNICEF Bw. Joseph Matimbwi akitoa mada katika kikao hicho amesema suala la Ukatili ni mtambuka hivyo jamii inapaswa kuungana hususani katika ukatili unaosababishwa na mitandao.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...