Njombe
Ili
kurahisisha huduma ya maombi ya umeme,shirika la umeme Tanzania
(TANESCO) limeanzisha na kuzindua huduma mpya ya maombi ya kuunganishiwa
nishati ya umeme kupitia simu zao.
Akizungumza
mara baada ya hafla fupi ya uzinduzi wa huduma hiyo inayoitwa Ni-Konekt
iliyofanyika katika viwanja vya polisi mjini Makambako mkoani
Njombe,Zaidat Ngoda afisa uhusiano wa huduma kwa wateja kutoka TANESCO
Makambako amesema huduma hiyo inakwenda kuwaondolea usumbufu wananchi
kufika ofisini kwa ajili ya maombi ya umeme.
“Kupitia
huduma hii mteja anapata huduma ya umeme popote pale alipo na hii
huduma inapatikana kwa njia nne kwa kumuangalia mwananchi yeyote mpaka
mwenye simu ndogo aweze kufanya maombi ya kuunganishiwa uememe lakini
njia nyinge ni ya kupitia tovuti ya WWW.TANESCO.CO.TZ” alisema Zaidat Ngoda
Amesema
ili kupata huduma hiyo kupitia simu ndogo ya kiganjani (kiswaswadu)
mteja ataweza kupata huduma hiyo kwa kwa kubonya *152* 00 na kasha alama
ya reli na kuendelea kufuata maelekezo huku kwa watumiaji wa simu janja
wataweza kupakua application inayoitwa Ni-Konekt ambayo ina maelezo
ndani ya maombi ya huduma ya umeme.
Nolasco
Mlowe ni diwani wa kata ya mji mwema aliyefika katika uzinduzi wa
huduma hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa
Makambako,amesema mfumo huo utawasaidia sana wananchi kwa kuwa awali
walikuwa wakipata taabu ya kufuatilia ofisi za TANESCO badala ya
kuendelea na shughuli zao.
“Awali
kulikuwa na hatua nyingi mpaka kwenda kwenye ofisi zao tu na mizunguko
mingine mingi lakini mfumo huu unaweza ukalipia kila kitu ukiwa nyumbani
kwako na kufungiwa umeme hivyo unapunguza muda nan i mfumo salama zaidi
wa kuepukana na matapeli”Amesema Mlowe
Aidha ametoa wito kwa TANESCO kuendelea kutoa elimu kwa shirika la umeme ili huduma hiyo iweze kuwafikia wananchi.
Nao
baadhi ya wananchi wa Makambako waliojitokeza katika hafla hiyo
wamepongeza shirika la Umeme kwa kuendelea kuwajali na kuzidi
kuwarahisishia huduma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...