Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekutana na kuzungumza na Uongozi wa Umoja wa Watu wenye Ulemavu waendesha Bajaji kutoka Mkoa wa Dar es Salaam (UWAWABADA) wametembelea katika ofisi yake jijini Dodoma kwa lengo la kubadilishana mawazo na kujadiliana kwa pamoja changamoto mbalimbali zinazowakabili katika sekta hiyo.

Aidha, Katika kikao hicho viongozi hao na wajumbe wa UWAWABADA wametoa pongezi zao kwa Waziri pamoja na Ofisi yake kwa namna wanavyo shughulikia masuala mbalimbali yanayowakabili Watu wenye Ulemavu ili kuimarisha ustawi wa kundi hilo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Viongozi wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu waendesha Bajaji Mkoa wa Dar es Saalam (UWAWABADA) walipomtembelea katika ofisi yake iliyopo Jengo la OSHA Jijini Dodoma, Juni 28, 2022.
Baadhi ya Viongozi na Wajumbe wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu waendesha Bajaji Mkoa wa Dar es Saalam wakisikiliza maelezo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (hayupo pichani).
Mwenyekiti wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu waendesha Bajaji Mkoa wa Dar es Saalam (UWAWABADA), Bw. Paul Majige akieleza jambo wakati wa kikao hicho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako walipomtembelea katika ofisi yake iliyopo Jengo la OSHA Jijini Dodoma, Juni 28, 2022.
Mjumbe wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu waendesha Bajaji Mkoa wa Dar es Saalam (UWAWABADA), Bi. Evodia Nchimbi akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Katibu wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu waendesha Bajaji Mkoa wa Dar es Saalam (UWAWABADA), Rebman Materu akifafanua jambo wakati wa kikao hicho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako walipomtembelea katika ofisi yake iliyopo Jengo la OSHA Jijini Dodoma, Juni 28, 2022.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...