Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU
wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ameagiza viongozi wa kata ya
Kikongo kushughulikia changamoto za migogoro ya ardhi na kusisitiza
endapo atabaini kuna mtu mbabaishaji basi atashughulika naye.
Alitoa
agizo Hilo wakati wa ziara ya kuzungumza na Wananchi wa Kata ya
Kikongo na kusikiliza changamoto iliyopo ya migogoro ya ardhi kati ya
wawekezaji na wanachi wa kata hiyo
Alieleza kuwa, Kata hiyo inadaiwa kuwa na changamoto na migogoro ya ardhi suala ambalo linapaswa kutafutiwa ufumbuzi.
Aidha, ameagiza shamba ambalo halina mgogoro shamba namba 30/1 liendelezwe
"kuna mashamba mawili moja lina mgogoro na lingine halina mgogoro
kwanini ambalo halina mgogoro lisiendelezwe."
alisema Kunenge.
Mkuu huyo wa mkoa amesisitiza viongozi washughulikie haraka shamba lenye mgogoro ili wawekezaji waendelee na shughuli Yao.
"Baadhi
ya viongozi acheni ubabaishaji,na nahimiza, suala la haki !!!"Mwenye
haki apewe ama mwananchi ana haki apewe haki yake na kama muekezaji
ana haki apewe haki yake." alieleza Kunenge.
Vilevile,Ofisa
Ardhi Grayson Gipson aliombwa kutoa mrejesho uliotolewa kipindi cha
Waziri wa nyumba, Maendeleo na Makazi William Lukuvi kwenye ziara
yake aliyofanya Julai 2021, ambapo alielekeza kuhusu mashamba mawili
yanayomilikiwa na Trans continental, la Kwanza ni 30/1 na la pili ni
30/2.
Ofisa
ardhi huyo, alieleza kuwa shamba namba 30/1 halina changamoto hivyo
kampuni ipo tayari kwa kufanya vipimo na kushughulikia shamba namba
30/1.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...