Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 25, 2022 ameitisha kikao cha kujadili utelekezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa jijini Dodoma la kuitaka Ofisi ya Waziri Mkuu itafute eneo jingine utakapojengwa mnara mpya wa mashujaa wenye hadhi ya Makao Makuu ya nchi.
Pichani, Mheshimiwa Majaliwa akiongoza kikao hicho kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene na kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...