ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa Al Ahly S.C., Pitso Mosimane amefika kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam kwa ajili ya Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea kilele cha Siku ya Mwananchi, Agosti 6, 2022 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mosimane ni Kocha aliyeiwezesha Al Ahly kutwaa ubingwa wa Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili mfululizo, atahudhuria siku ya kilele cha Siku ya Mwananchi.

“Nimevunja mkataba na Al Ahly SC ili nipumzike, nimeamua kuja nchini Tanzania kupata mapumziko, nimekuja hapa nchini mara nne sikuiona hii nchi vizuri, mara nyingi nimefika uwanja wa ndege na kuingia uwanjani kwenye mashindano.” Amesema

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...