*Ni kauli ya msisitizo iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akiwaambia wavamizi wa ardhi, asema kinachofuata hapo ni mazungumzo tu

Na MWANDISHI WETU

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Amos Makala amesema mvamizi yeyote wa ardhi ambaye hana karatasi au hati miliki ya ardhi hana haki na kuwa kinachofuata baada ya hapo ni mazungumzo tu.

“Bila karatasi wala hati huna haki, kinachofuata baada ya hapo ni mazungumzo tu kwani mvamizi ni sawa na mhalifu,” alisema Mhe. Makala wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mabwepande Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mhe. Makala alisema mvamizi yeyote ni sawa na mhalifu na kwamba mbele ya Sheria makosa hayo ya uvamizi wa ardhi ni sawa na kosa la jinai hivyo mtu anapoelekezwa kuwa makosa yamefanyika na anatakiwa awe mwepesi wa kuunga mkono na kurekebisha makosa kwani wakiendelea na ubishi hautawasaidia.

“Nimekuja na watu wa NSSF lile eneo lao wanapima viwanja na nimewaambia wapime viwanja rafiki ili watu wa Mabwepande nao waweze kupata,” alisema.

Alisema wameanza kupima katika eneo la NSSF na baadaye wataenda katika eneo la DDC na eneo la Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo yamevamiwa pamoja na taasisi nyingine zote ambazo zimevamiwa.

Mhe. Makala alizitaka taasisi zote ambazo zinamiliki maeneo katika Kata hiyo ya Mabwepande kutenga maeneo kwa ajili ya huduma mbalimbali za jamii kama ambavyo NSSF walishafanya kwa kutoa eneo kwa ajili ya kujenga shule.

Naye, Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Songoro Mnyonge aliupongeza Mfuko wa NSSF kwa kukubali kupanga upya eneo lao na pia kutoa eneo ambalo litajengwa Shule.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Godwi Gondwe alisema katika eneo la NSSF limeshapimwa na limeshawekwa alama jambo ambalo litaondosha uvamizi wa ardhi katika eneo hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Amos Makala,  akizungumza na baadhi ya wakazi wa Kata ya Mabwepande
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Godwin Gondwe, akizungumza na baadhi ya wakazi wa Kata ya Mabwepande
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Songoro Mnyonge akizungumza wakati wa mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makala uliofanyika katika Kata ya Mabwepande
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makala akitoa maelekezo kwa taasisi mbalimbali ambazo zinamiliki ardhi katika kata ya Mabwepande. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi Gabriel Silayo.
Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Kanda ya  Dar es Salaam Idrisa Kayera , akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo kuhusu ardhi wakati wa Mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makala na wakazi wa Mabwepande
Matukio mbalimbali katika picha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...