Na Mwandishi Wetu
ALIYEKUWA Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam Suleimani Kova anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Mtandao wa Wasanii wanawake Tanzania 'Ladies Faaa' unaotarajia kufanyika Agosti 19 chuoni Splendid Ilala jijini humo.

Akizungumza jana, Katibu wa mtandao huo Asha Salvador alisema uzinduzi huo utasindikizwa na burudani kutoka kundi la Safi.

Salvador alisema uzinduzi huo utahudhuriwa na wadau zaidi ya 80 ambao wataunganisha nguvu ya pamoja itakayosaidia maendeleo.

Aidha Salvador alitumia fursa hiyo kuifafanua taasisi hiyo inayopinga unyanyasaji wa kijinsia kwa vijana wa kike na kiume sambamba na akina mama, elimu itakayotolewa mashuleni na mtaani.
Mkurugenzi wa Mtandao wa Wasanii wanawake, Anifa Taalib
Katibu wa mtandao wa Wasanii wanawake, Asha Salvador

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...