Na Jane Edward, Arusha
Watafiti kutoka Kituo cha utafiti cha Tari Seliani wameanza kuyaongezea thamani maharage ya Jesca kutokana na madini chuma na Zinki yaliyopo kwenye maharage hayo kwa kutengeneza aina mbalimbali za vyakula vinavyotokana na maharage hayo.
Hayo yamebainika wakati wa maonyesho ya wakulima na mifugo nanenane yanayofanyika kwa kanda ya kaskazini ikijumuisha mikoa ya Kilimanjaro,Tanga,Manyara na Arusha ambao ndiyo wenyeji wa maonyesho hayo.
Aidha watafiti hao wanasema katika kuongezea thamani maharage hayo ya Jesca kwa sasa wameweza kutengeneza Biskuti,Keki na Mikate inayotokana na maharage hayo ili kuendelea kuupa thamani unga huo.
Salome Munis ni mtafiti muandamizi kutoka Tari Seliani ambapo anasema maharage hayo yanaweza kubadilisha maisha ya watanzania kuweza kuacha kutumia vyakula vyenye wanga na badala yake kutumia vyakula vyenye protini zaidi ikiwemo maharage hayo.
Akiainisha baadhi ya aina ya mazao waliotafiti amesema Kwa sasa mbali na maharage ya Jesca pia wametafiti mazao ya ngano, shayiri ambayo yameweza kupokelewa vizuri na jamii.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliotembelea Banda la Tari Felista Madon wamepongeza hatua hiyo kwa kuwa hawatakuwa na changamoto ya utumiaji vyakula vya wanga.
Wakazi wa Kanda ya kaskazini wameendelea kutembelea maonyesho ya kilimo na mifugo kujionea bidhaa mbalimbali kwenye maonyesho hayo yenye kauli mbiu kilimo ni biashara,shiriki kuhesabiwa kwa mipango bora ya kilimo,mifugo na uvuvi.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...