Njombe
MWALIMU Betrece Mtweve wa shule ya msingi Ngalawale iliyopo Ludewa kijijini mkoani Njombe ameiomba serikali iwasaidie kujenga barabara katika maeneo yao hususani kuelekea katika shule yao kwa kuwa wamekuwa wakitamani kununua magari kama watu wengine lakini wanashindwa kutokana na kukosa barabara ya kupitisha usafiri.

Mwalimu Betrece amebainisha hilo wakati wa mafunzo ya makarani wa sensa ya watu na makazi walipotembelewa na mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga wilayani hapo ili kuona maendeleo ya mafunzo na kusikiliza changamoto zao.

“Ombi langu kubwa ni barabara,yaani hadi nashindwa kununua gari kwasababu ya barabara mfano kutoka kwenye barabara kuu hadi kuingia shuleni kwangu hususani kipindi cha mvua siwezi kuingia hata kwa pikipiki”amesema Mwalimu Mtweve

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...