Na John Walter-Manyara.


Mganga Mkuu wa serikali Dr.Aifello Sichwale amewatoa hofu watanzania juu ya taarifa za uwepo wa ugonjwa wa homa ya nyani katika maeneo mbalimbali duniani ambapo amesema hadi sasa hakuna mgonjwa wa homa hiyo hapa nchini.

Akizungumza na wataalamu wa afya wilaya ya Babati mkoani Manyara Dr. Sichwale amesema kumekuwa na maswali mengi yanayoonyesha hofu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa homa ya nyani,ambapo amesema serikali inafuatulia kwa ukaribu taarifa za Kila mgeni anayeingja nchini.

Amesema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo ufuatiliaji wa wasafiri wanaoingia nchini kupitia vituo vyote vya mpakani na tayari watumishi wamepatiwa mafunzo ya utambuzi wa ugonjwa huo.

Ugonjwa wa homa ya Nyani husababishwa na wanyama aina ya Nyani na Panya ambapo mgonjwa huwa na mwonekano wa malengelenge hasa maeneo ya mkono yanayofanana na ugonjwa wa Tetekuwanga.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...