Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekemea tabia ya udhalilishaji inayodaiwa kufanywa na baadhi ya watumishi waliopewa dhamana katika halmashauri mbalimbali ikiwemo ya Sikonge.

Akizungumza leo Agosti 18, 2022 wilayani Sikonge, Mkoa wa Tabora akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Uhai wa Chama mkoani Tabora, amesema Chama hakiungi mkono udhalilishaji wowote na inafuatilia hatua kwa hatua jambo hilo.

“Nataka niseme na hili la udhalilishaji wanawake kingono, nimelikuta Kaliua na lipo Sikonge, lakini hata kwenye maeneo mengine kwa watumishi wa umma, ujumbe umefika, wenye hiyo tabia waache, waache kuwadhalilisha dada zetu, waache kuwadhalilisha mama zetu, waache kuwadhalilisha ndugu zetu wa kike hapa Sikonge, hiyo tabia imeshamiri kwa sababu tu kuna mtu anadhamana, ana fursa ya kuwasaidia wengine.

“Hamuwasaii mama zetu, hamsaidii dada zetu mpaka muwadhalilishe kingono, Chama kinafuatilia kwa karibu sana, hataturahusu udhalilishaji wa aina yoyote kwa wanawake ndani ya nchi hii, wanawake hawa wanauwezo mkubwa sana katika kufungua fursa za maendeleo katika taifa letu.

“Wakithubutu akina mama wanaweza, hatuwezi kuacha uthubutu wao kwa sababu tu sisi akina baba baadhi yetu tunashindwa kuzuia hisia zetu, tena sio kushindwa kuzuia hisia zetu ila hatuna adabu tu, ni utovu wa adabu tuliokuwa nao,” 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...