Na Pamela Mollel,Arusha

Taasisi ya Uhandisi na usanifu mitambo Tanzania (TEMDO)wabuni mtambo mpya wa kuchakata mafuta ya Alizeti yenye uwezo wakusafisha mafuta lita 1000 kwa siku

Akizungumza na vyombo vya habari katika maonesho ya nane nane jijini Arusha,Mkuu wa kitengo cha mawasiliano na masoko Dkt Sigisbert Mmasi alisema kuwa mtambo huo utakwenda kuwasaidia wajasiriamali kuboresha bidhaa zao ili kuendana na soko

Alisema kuwa mtambo huo wa kuchakata na kusafisha mafuta ya alizeti ni kivutio kikubwa katika maonyesho hayo huku akitaka wajasiriamali kuchangamkia fursa hiyo

"Awali kabla ya uwepo wa mashine hicho kulikuwepo na changamoto ya kusafisha mafuta hali iliyowalazimu wajasiriamali kuingia gharama kubwa kusafisha mafuta katika viwanda vikubwa"alisema Dkt Mmasi

Mbali na uwepo wa Teknolojia hiyo ya mashine ya kuchakata Alizeti pia TEMDO wana mashine mbalimbali ikiwemo ya kutengeneza siagi ya karanga,mashine ya kuchakata unga lishe na viungo vya kupigia,mashine ya kuchakata zao la muhogo na sukari Pia wanatengeneza vifaa tiba kama vile vitanda vya kujifungia wamama wajawazito.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...