Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imefanya kikao cha Baraza la
wafanyakazi leo ili kujadili mafanikio, mafanikio, changamoto na njia za kuweza
kutatua changamoto zilizojitokeza wakati wa bajeti mwaka uliopita ya 2021/2022.
Akizungumza kwenye kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Wataalamu Ununuzi na Ugavi Godfred Mbanyi amesema baraza ni chombo kinachoundwa na
sheria ya Mahusiano kazini kwa ajili na kuweka mazingira mazuri mahali pakazi ambapo
chombo hiki kinawiwa kwa mkataba baina na Menejimenti pamoja na chama cha
wafanyakazi sehemu ya kazi.
Pia amasema baraza la leo limefanyika ili kutathmini
utendaji kazi wa bajeti ya mwaka uliopita ya 2021/2022, kisheria na kiutaratibu
bajeti yoyote kabla haijahidhinishwa lazima ipitishwe na Balaza la Wafanyakazi
sehemu ya kazi.
Mbanyi amesema Bajeti ya mwaka 2021/2022 ilikamilika toka
Juni 30 hivyo ni wajibu wa menejimsenti kuja kueleza balaza nini mafanikio,
changamoto na njia za kuweza kutatua
changamoto zilizojitokeza wakati wa bajeti iliyokamilika muda wake.
“Umuhimu wa Mabaraza ya kazi kwanza yanaleta ushirikishwaji
wa wafanyakazi sehemu ya kazi hivyo wafanyakazi wanakuwa ni sehemu ya maamuzi katika
taasisi, kwaiyo taasisi sio kwamba inakuwa inaongozwa na Menejimenti lakini
inakuwa na chombo ambacho kinawakilisha wafanyakazi wote katika taasisi mbalimbali.”
Alisema Mbanyi
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) Godfred Mbanyi akizungumza wakati wa kufungua kikao cha baraza la wafanyakazi wa PSPTB likilokuwa na lengo la kutathimini Utendaji kazi wa Bodi hiyo lililofanyika leo Bagamoyo.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Taaluma wa PSPTB Amos Kazinza akitolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya hoja zilizokuwa zinatolewa na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa PSPTB wakati wa kikao kilichofanyika Bagamoyo Mkoani Pwani leo.
Kaimu Mkurugenzi wa mafunzo wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) , Amani Ngonyani akijibu hoja za wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa PSPTB ili kuboresha Utendaji kazi wa Bodi hiyo kwenye kikao cha Baraza hilo kilichofanyika Bagamoyo Mkoani Pwani.
Katibu mkuu wa TUGHE Taifa, Hery Mkunda akitoa salamu za uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania ( TUGHE ) wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa PSPTB likilokuwa na lengo la kutathimini Utendaji kazi wa Bodi hiyo lililofanyika leo Bagamoyo.
Mwenyekiti wa TUGHE PSPTB, Shilla Mwandu( wa kwanza kushoto) akizungumza kuhusu namna wafanyakazi wanabidi kujitadhmini pale wanapokuwa wanafanya kazi za Serikali wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa PSPTB lililofanyika Bagamoyo mkoani Pwani.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa PSPTB wakifuatilia mada zilizokuwa zinawasilishwa kwenye kikao kazi kilichokuwa na lengo la kutathimini Utendaji kazi wa Bodi hiyo lililofanyika leo Bagamoyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Bodi hiyo pamoja na wageni waalikwa wakati wa wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa PSPTB likilokuwa na lengo la kutathimini Utendaji kazi wa Bodi hiyo lililofanyika leo Bagamoyo mkoani Bagamoyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...