Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na walimu namna ambavyo ukatilii wa kingono unavyokuwa kwa kasi baina ya walimu na wanafunzi

Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami akiongea jambo na Mwenyekiti wa Chama cha waalimu Mkoa wa Iringa Mwalimu Stanslaus Muhongole wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho wilaya ya Iringa Vijijini

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongongozwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami kutoka kwenye mkutano huo mara baada ya kumaliza kuhutubia

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akipokea hotuba ya walimu wa Iringa Vijijini wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho.


Na Fredy Mgunda,Iringa.

CHAMA Cha Walimu Wilaya ya Iringa vijijini (CWT) kimeonya kuwa hakitohusika na utetezi Wa Waalimu watakaojihusisha na vitendo vya utovu Wa nidham ikiwemo mahusiano ya kingono na wanafunzi.

Mwenyekiti Wa CWT Wilaya ya Iringa Vijijini Mwalimu Simoni Mnyawami amesema ni aibu kusikia waalimu wakitajwa kuhusika uhalifu huo huku akisisitiza hatua zaidi za kisheria zichukuliwe ili iwe fundisho Kwa watakaobainika.

Mwenyekiti huyo ameyasema hayo wakati wa mkutano mkuu wa CWT baada ya Mgeni wa Heshima mkuu wa wilaya ya Iringa kuwataka waalimu kuzingatia weledi wa taaluma kwa kuwafifichua wanaojihusisha kingono na wanafunzi.

Mnyawami alisema kuwa suala la utovu wa nidhamu linapaswa kuheshimuwa kwa kila mwalimu ili kulinda hadhi ya taaluma hiyo Ikiwemo Utoro, ulevi wa kupindukia pampja na baadhi ya waalimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi.

Mwenyeji wa Mkutano Huu mkuu wa kikatiba Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami alisema ni muhimu waalimu akatambua na kuheshimu taaluma waliyo nayo Kwa kuwa wamepewa dhamana na serikali pamoja na jamii kuwa walezi wa watoto katika kuwajenga kinidham na kitaaluma

Kulingana na Changamoto ya utovu wa nidham unaotajwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo aliyekuwa Mgeni wa heshima anasema jambo la walimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi halipaswi kufumbiwa macho

Moyo amewataka walimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wanaowafundisha ili taifa liweze kupata wasomi wengi ambao wanauwezo wa kuja kukisaidia Taifa hapo baadae.

Alisema kuwa Kuna baadhi ya walimu wamekuwa wakiaribu taswira halisi ya kada ya ualimu kwa baadhi ya walimu kufanya mapenzi na wanafunzi na uwafanyia ukatili wanafunzi kwa makusudi hivyo walimu wanapaswa kutoa taarifa kwa mwalimu yeyeto atakayekutwa anafanya vitendo vya ukatili.

Alisema kuwa kazi kubwa ya mwalimu ni kuwafundisha wanafunzi waweze kufaulu na sio kuwafanyia ukatili wanafunzi..

Aidha Moyo alimazia kwa kusema kuwa walimu wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa wamekuwa wanafanya vizuri kwenye kufundisha wanafunzi ndio maana matokeo yake yamaekuwa mazuri mwaka hadi mwaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...