Njombe

Katibu mkuu wa wizara ya Katiba na Sheria nchini Bi.Merry Makondo amesema serikali ya Tanzania inakwenda kufanya mapitio ya mfumo wa haki jinai nchini ili kuhakikisha mashauri yote yanafanyiwa upelelezi kwa haraka ili kuzisaidia Mahakama kuharakisha uendeshaji wa kesi na kutoa haki kwa wakati.

Amebainisha haya mkoani Njombe kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Dkt,Damas Ndumbaro wakati wa maadhimisho ya miaka 27 ya kituo cha sheria na haki za binadamu.

“Serikali inaenda kufanya mapitio ya mfumo wa haki jinai nchini kuhakikisha kwamba mashauri yote ya jinai katika ngazi ya uchunguzi,upelelezi,uendeshaji wa mashtaka,utoaji wa ushahidi pamoja mashauri yanavyosikilizwa uweze kuboreshwa na kuaptiwa ufumbuzi kwa haraka”amesema Bi.Makondo

Katika kuhitimisha zoezi la utoaji wa msaada wa kisheria katika nyanja mbali mbali kupitia kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) uliofanyika mkoani Njombe wakati wa kuadhimisha miaka 27 ya kituo hicho,Mkurugenzi wa kituo Bi.Anna Henga amesema wananchi 796 wamehudumiwa moja kwa moja na mawakili wa kituo wakati wa maadhimisho.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...