Njombe

Mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa ametoa wito kwa watu wanaoishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi kuacha kuogopa kutumia dawa za kufubaza maambukizi kwa kuwa serikali imetatua changamoto ya kukosekana kwa dawa hizo huku akiwataka kuacha kuchanganya ARV's na dawa za kienyeji.

Aidha mkuu huyo wa wilaya mara baada ya kukagua shughuli za maendeleo zinazofanywa na vikundi vya WAVIU kupitia konga za halmashauri ya wilaya ya Njombe,amesema ni hatari kwa watu kunywa dawa kwa kificho kwa kuwa wamekuwa wakijisababishia matatizo makubwa.

“Ukiacha dawa ghafla kuna madhara makubwa na wengine wanachanganya na dawa za kienyeji,lakini kuna hawa wanaokunywa dawa kwa kificho hii ni hatari zaidi kwasababu unapoenda kliniki unapimwa na wataalamu wanajua kama kuna haja ya kukubadirishia dawa,wengine wamefikia hatua ya kununua wenyewe dawa za nje zisizokuwa na kipimo na kupata madhara”amesema Kissa Kasongwa

Mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Dkt,Suke Magembe ametoa ushauri kutumiwa dawa zilizothibitishwa na mkemia mkuu ili kuepukana na madhara.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...