Na. OMM Rukwa
MKUU wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga ametoa wito kwa wananchi kutowaficha ndani watoto wanaostahili kupewa chanjo ya polio ili kuwakinga na ugonjwa wa ulemavu.

Ametoa agizo hilo leo (01.09.2022) wakati akizindua kampeni ya tatu ya utoaji chanjo ya polio Kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano iliyofanyika kimkoa katika Kituo cha Afya Mazwi kilichopo Manispaa ya Sumbawanga.

Sendiga aliongeza kusema chanjo ya polio inayotolewa ni salama na kuwa serikali imejipanga kuhakikisha watoto wanakuwa na afya njema.

" Wito wangu ni kwa akina mama na akina baba kujitokeza na kushiriki kutoa taarifa za watoto wanaostahili kupata chanjo ili wataalam wa afya wawafikie huko majumbani na kuwapa chanjo ya polio" alisema Sendiga.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryuba alisema Wilaya yake imejipanga kuhakikisha watoto wote wanaostahili wanafikiwa majumbani ndani ya siku nne za kampeni hii ya polio.

Waryuba alisema katika kampeni hii ya awamu tatu Halmashauri ya Manispaa imelenga kuchanja watoto 51,919 na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga itachanja watoto 83,573.

Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Ibrahim Isaack alisema kampeni hii ya tatu Mkoa umelenga kutoa chanjo ya Polio kwa watoto 276,320 kuanzia tarehe 01 hadi 04 Septemba 2022.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...