Afisa Mkuu wa Kodi Bw.  John Kabuteni akitoa Elimu ya Kodi kwa wafanyabiashara wa Bariadi mjini Mkoani Simiyu.


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) leo imeanza kampeni yake Elimu ya mlango kwa mlango katika mkoa wa Simiyu wilaya ya Bariadi yenye lengo la kuelimisha wafanyabiashara wa Bariadi juu ya masula mbalimbali ya Kodi sambamba na kusikiliza changamoto za wafanyabiashara hao ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

Mkuu wa wilaya ya Bariadi Bw. Lupakisyo Kapange kabla ya kuanza kwa Kampeni hiyo, amesema amefurahishwa na ujio wa Maafisa hao kuwataka wafanyabiashara wa wilayani hapa kuwapa mashirikiano maafisa hao watakapo watembelea maduaka yao pia kutumia furasa hiyo kuuliza maswala na kutoa maoni yao. 

“Nawashukuru maafisa wa TRA kwa kuja kutetembelea katika kipindi hiki ambapo wilaya ya Bariadi imekua ikipiga maendeleo makubwa na matumaini yake baada ya zoezi hili la kungea kirafiki litawahamisiha kuendelea kulipa kodi zaidi”.

Aidha amewasisitiza pia wafanyabiashara wa Wilaya hio inayoongoza kwa makusanyo katika mkoa wa Simiyu kuendelea kulipa kodi kwa hiari bila ya kushurutishwa ili kuweza kuisadia serekali kukamilisha miradi ya kuwaeletea maendeleo ya nchi yetu sambamba na hilo amewakumbusha wafanyabiashara kuendelea kutoa risiti kila wanapuza bidhaa au kutoa huduma na wananchi kudai risiti kila wanaponunua bidhaa.  

Aidha kwa upande wa Afisa wa Kodi kutoka kitengo cha Elimu na Huduma kwa Mlipa kodi mkoa wa Simiyu, Bw. Benjamin Makobwe ameeleza lengo la Kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara na kusikiliza changamoto zao hivyo amewataka wafanya biashara wawepe ushirikiano ili kufikia lengo la zoezi hilo.

“ leo tupo hapa mkoa wa Simiyu wilaya ya Bariadi kwa lengo la kuelimisha wafanyabiashara wa eneo  hili masuala mbali mbali ya kodi pamoja kusikiliza changamoto na madukuduku yao kwa lengo kuyafanyia kazi”.

Kwa upande wao wafanyabiashara wa wilaya hio wamefurahishwa sana na kuwapngeza maafisa wa TRA kwa kufika katika wailaya ya Bariadi kwa lengo la kuwapatia elimu zaid katika masuali ya Kodi sambamaba na hilo walitoa wito kwa wafanyabiashara wengine kutoa ushirikiano kwa maafisa hao na kuwaahimiza wafanyabiashara kutoa risiti halali za EFD kila wanapouza na wananchi kudai risiti ili kuiwezesha serekali kukusanya kodi ambayo ndio inayotumika kujenga mashule, vituo vya afya, barabara na usamabazaji wa maji mijini na vijijini.

‘Nifurahishwa sana na ujio wa maafisa wa TRA kwanza tumekuwa nao kama familia mja ukiwa na familia ya upendo kama tulivyosasa sisi na TRA tutaweza kurahisisha ukusanyi wa Kodi na kuiwezesha serikali kuleta maedndeleo zaidi”. Alisema Faida Jishiku (mfanayabiashara).

Kampeni ya Elimu ya mlango kwa mlango huendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) chini ya kitengo cha Huduma na Elimu kwa Mlipakodi  kwa kuwatembelea wafanyabiashara wa mikoa yote nchini kwa lengo kuwapatia elimu ya kodi pamoja kusikiliza changamoto zao pamoja na maoni na kuyafanyia kazi ili kujenga mahusiano mema na wafanyabiashara na kurahisisha ulipaji wa kodi bila ya kukwaruzana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...