Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu imepata ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar ambao umelenga katika kubadilishana uzoefu katika masuala ya kazi, maendeleo vijana, ukuzaji ajira na ustawi wa Watu wenye Ulemavu.

 Ugeni huo umeongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais anayesimamia masuala ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji. Katika kikao hicho ofisi hizo zimedhamiria kushirikiana kwa karibu katika kutekeleza majukumu sambamba na kutoa huduma kwa wananchi kwa tija na ufanisi katika pande zote mbili za Muungano.

 

Aidha, katika kikao kazi hicho Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Kazi, Uchumi na Uwekezaji aliambatana na Kamishna wa Kazi – Zanzibar pamoja na Mkurugenzi wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSH) – Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Dkt. Islam Salum akizungumza wakati wa kikao cha Ushauriano baina ya ofisi hiyo na Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Oktoba 13, 2022 Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma. Kikao hicho kililenga kujadili utekelezaji wa shughuli zinazotekelezwa na ofisi hizo kwa pande zote mbili.

Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Dkt. Islam Salum wakati wa kikao cha Ushauriano baina ya ofisi hiyo na Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Oktoba 13, 2022 Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Bw. Leonard Mchau (kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Ushirikiano baina ya ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar kilichofanyika Oktoba 13, 2022, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Bw. Leonard Mchau (kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Ushirikiano baina ya ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar kilichofanyika Oktoba 13, 2022, jijini Dodoma.
Kamishna wa Kazi Msaidizi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Bi. Lilian Francis (kushoto aliyesimama) akiwasilisha taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Idara ya Kazi wakati wa kikao cha Ushirikiano baina ya ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar kilichofanyika Oktoba 13, 2022, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Kitengo cha Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Bw. Rashid Maftah (kulia) akiwasilisha taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na kitengo hicho wakati wa kikao cha Ushirikiano baina ya ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar kilichofanyika Oktoba 13, 2022, jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...