Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Anthony Mavunde amezitaka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Kilimo kuhakikisha zinayapima maeneo yao ili kupata hati za umiliki wa ardhi na pia kuweka uzio katika maeneo yote ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima na kupunguza uvamizi wa maeneo hayo.

Naibu Waziri Mavunde ameyasema leo mkoani Mwanza wakati wa kikao cha utatuzi wa migogoro ya ardhi ya Vijiji 975 inayoshughulikiwa kamati ya Mawaziri nane wa kisekta ambapo leo kamati hiyo ilikuwa katika Kata ya Shibula,Wilaya ya Ilemela-Mwanza.

“Ni wakati muafaka sasa Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya kilimo kuhakikisha mnayalinda na kuyatunza maeneo yenu kwa kuyapima na kuzungushia uzio.

Kuyaacha mashamba haya bila kuyatumia kwa eneo kubwa kunasabisha uvamizi wa maeneo haya ambayo mengi yametengwa kwa ajili ya uzalishaji mbegu na utafiti wa kilimo.

Hivyo naagiza Taasisi zote kuhakikisha mnatenga bajeti ya kulinda haya maeneo na kusimamia malengo ya matumizi yake,Mh.Rais Samia Suluhu Hassan ametuongezea bajeti kwenye wizara yetu hivyo hakikisheni katika mipango yenu inahusisha ulinzi wa maeneo haya”Alisema Mavunde

Katika zoezi hili jumla ya hekta 92 zilizopo katika eneo la Taasisi ya Utafiti ya Kilimo Ukiriguru zimegawiwa kwa wananchi ili kuruhusu shughuli za kilimo zinazofanywa na wananchi katika eneo hilo kama njia ya utatuzi wa mgogoro huo.

 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...