NaFaustine Gimu,Bugango Uganda/Tanzania .
BAADHI ya raia wa Uganda wamesema ushirikiano na ujirani mwema Tanzania umekuwa nguzo muhimu katika kupambana na ugonjwa wa Ebola kwa kuweka mikakati ya pamoja katika kuzingatia kanuni za afya hasa mipakani.

Wakizungumza katika kijiji cha Bugango upande wa Uganda,baadhi ya raia wa Uganda akiwemo Mulikatete Jesca pamoja na Gaspary Kundii wamesema hatua hiyo ya ujirani mwema imekuwa ni msingi mkubwa kwa kusaidiana masuala mbalimbali ikiwemo ikiwemo hatua za kuzingatia kupambana na Ebola.

“Sisi na Tanzania tunaujirani mwema hatuna shida yoyote ,tunapoenda Tanzania tunahudumiwa ,tunanawa na Jick [sanitizer],tunapewa huduma zote za afya bila shida yoyote “amesema Mulikatete.

Nao baadhi ya viongozi wa kijiji cha Bugango kwa upande wa Tanzania akiwemo mwenyekiti wa kijiji Meshack Masumbuko pamoja na mtendaji wa kijiji Anthony Jovenary wamesema wamekuwa na mkakati wa kuitisha mikutano ya pamoja kwa pande zote kwa ajli ya kuwekeana taratibu za kuzingatia kanuni za afya hali ambayo imesaidia kanuni za afya kuzingatiwa mipakani

Kwa upande wake Mganga mkuu mkoa wa Kagera .Dkt,Issessanda Kaniki amesema wameweka mbinu ya pamoja katika utoaji wa huduma na ufuatiliaji wa pamoja tetesi za wahisiwa wa Ebola na ukaguzi wa wasafiri kwa pande zote mbili.

“Tunashirikiana kuweza kutoa taarifa na kutoa huduma iwapo mtu atatokea”amesema Dkt.Kaniki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...