Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko leo tarehe 1 Oktoba, 2022 ametembelea banda la NSSF katika Maonesho ya Tano ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya uwekezaji (EPZA)Bombambili Mkoani Geita.
 
Ambapo aliupongeza Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) unavyohakikisha unatekeleza mpango wake wa kuyafikia makundi mbalimbali wakiwemo wachimbaji wadogowadogo wa madini katika maeneo mbalimbali.


Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF,Lulu Mengele akitoa maelezo kwa Waziri wa Madini, Mhe.Dotto Biteko leo 1 Oktoba, 2022 wakati alipotembelea banda la NSSF kwenye Maonesho ya Tano ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya uwekezaji (EPZA)Bombambili Mkoani Geita.

NSSF inashiriki Maonesho hayo kwa lengo la kutoa huduma mbalimbali za Hifadhi ya Jamii kwa wanachama na wananchi ikiwa pamoja na kusajili wanachama wapya wanaofika katika Banda la NSSF.
 
 


 


 

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...