Na Mwandishi Wetu

Msimu huu kazi ipo! Mabingwa mara tano wa Michuano ya Kombe la Dunia, timu ya taifa ya Brazil imeanza rasmi Michuano hiyo ya mwaka 2022 inayoendelea nchini Qatar baada ya ushindi mabao 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya Serbia.

Katika mchezo huo wa Kundi G, mabao ya ‘A Seleção’ yote yamefungwa na Mshambuliaji, Richarlison de Andrade kwenye dakika ya 62’ na 73’, Mshambuliaji huyo anacheza katika Klabu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza.

Wababe hao wa Soka la Dunia wakiongozwa na Kocha wao Tite wakiwa na Nyota wao maarufu duniani, kina Neymar, Vinicius Jr, Raphinha, Casemiro, Alex Sandro, Marquinhos Thiago Silva, Golikipa Alisson aliwanyanyasa vilivyo Serbia hususani kipindi cha pili.

Mabingwa hao wa Michuano hiyo, mwaka 1958, 1962, 1970, 1994 na 2002 kwa sasa wanaongoza Kundi G wakiwa na alama zao tatu sawa na Switzerland katika nafasi ya pili, huku Cameroon wakiwa nafasi ya tatu na Serbia wakiburuza mkia bila alama.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...