Na Khadija Seif, Michuzi TV
WASANII wa Filamu Mkoa wa Dar es salaam waongoza kwa kazi zao kupitia kwenye mchujo wa awali katika Msimu wa pili wa tuzo za Filamu za kitanzania unaotarajiwa kufanyika Disemba 17,2022 Jijini Arusha

Akizungumza na Wanahabari Novemba 29,2022 Jiji Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa bodi ya Filamu Dkt. Kiagho Kilonzo amesema kutokana na Makongamano pamoja na Semina mbalimbali ambayo yanafanyika kwa baadhi ya mikoa huku akiitaja Geita,Mbeya na Mkoa wa Dar es salaam imesaidia kwa kiasi kikubwa kukidhi kwa baadhi ya kazi kuingia kwenye mchakato wa awali wa kushindania tuzo za Filamu nchini.


"Tumebaini kuwepo kwa changamoto ya baadhi ya mikoa kutopata elimu namna ya uandaaji wa kazi zao na namna gani zinaweza kuwa bora zaidi hivyo kwa mkoa wa Dar es salaam umeongoza kwa kazi 128 kuingia katika mchakato wa awali.

Hata hivyo Kiagho ameeleza kwa mwaka huu kumekuwa na mabadiliko na maboresha katika sehemu mbalimbali ikiwemo Kamati ya uratibu wa zoezi la kukusanya kazi iliweza kufika mikoa 25 ya Tanzania kukusanya kazi tofauti na mwaka jana 2021 kamati iliweza kuzunguka mikoa 7.


Aidha,Kiagho amefafanua zaidi Mkoa wa Dar es salaam ndio mkoa ulioongoza kwa kukusanya kazi 189 na filamu 127 zimeweza kukidhi vigezo huku Mkoa wa geita walikusanya kazi 9 na 4 kukidhi vigezo hivyo ikiwemo ubora wa picha, sauti, muongozo pamoja na mpangilio wa visa na matukio.


" Ni dhahiri kuwa makongamano yamekuwa na msaada tosha katika kuendeleza kuwapa msasa watayarishaji wa filamu na wasanii hususani kwa baadhi ya mikoa kupelekea kufanya vizuri kwa mchujo wa awali katika tuzo hizi ukiwemo mkoa wa Dar es salaam, Mbeya,Geita pamoja na Songwe."


Pia ameweka wazi mikakati ya bodi ya filamu kuhakikisha katika ukuaji wa sekta ya Sanaa itahakikisha watayarishaji na wasanii wanapewa semina mara kwa mara zitakazowajengea morali ya kufanya kazi zenye ushindani na zenye ubora wa Kimataifa.


Kwa upande wake Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Filamu Emmanuel Ndumukwa amefafanua zaidi kuwa baada ya zoezi la mchujo wa awali wa filamu zilizofanikiwa kuingia kwenye mchakato kukamilika kinachofata ni nafasi ya kuzitazama filamu 151 ,ambapo ndani ya filamu hizo jopo la majaji litafanya kazi ya kuchagua zipi zitapigiwa kura na mashabiki.


Hata hivyo Ndumukwa ameongeza kuwa filamu 60% zitapigiwa kura na jopo la majaji huku 40% zitapigiwa kura na watazamaji ambapo zitaonyeshwa chaneli ya sinema zetu 103 kuanzia Novemba 30,2022 .

"Kazi zitaanza rasmi kuonyeshwa leo Novemba 29,2022 hadi Disemba 08,2022 sambamba na jopo la majaji litakaa na kuchagua filamu zitakazoingia kwenye kinyang'anyiro cha tuzo katika vipengele mbalimbali kuelekea kilele chake Disemba 17,2022 Jijini Arusha "

Kwa upande wake Msanii wa filamu na mtayarishaji kutoka Mkoa wa Mbeya Pius Nyange amesema Bodi ya filamu imeendelea kuamsha ari kwa wasanii kufanya kazi zenye ushindani kutokana na kuwepo wadau mbalimbali wanaounga mkono sekta ya Sanaa kwa ujumla.

Nyange pia ametoa pongezi kwa jopo la majaji kwa kukamilisha mchujo huo wa awali ambapo amefanikwa kupitia na kazi zake 3 ikiwemo Kosa,Kiganja,Karamu.

Hata hivyo wasanii waliopita kwenye mchujo huo ni pamoja na Lucas Mhuvile joti akifanikiwa kuingiza kazi 5 ikiwemo
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Dkt.Kiagho Kilonzo akizungumza na waandishi wahabari na wadau wa Filamu nchini Jijini Dar es salaam na kutambulisha Filamu zilizofanikiwa kuingia kwenye mchujo wa awali wa filamu 187 ambazo zitaanza rasmi kuonyeshwa kwenye chaneli ya sinema zetu leo Novemba 29,29,2022 mpaka Disemba 08,20,2022 kuelekea kilele cha tuzo hizo Disemba 17,2022 Jijini Arusha
 Msanii wa vichekesho Lucas Mhuvile maarufu Joti akiuliza swali kwa kamati ya uratibu wa tuzo za Filamu nchini namna gani waliofanikiwa kuingia kwenye mchujo wa awali watapata nakala ya orodha ya kazi zao zilizofanikiwa kupita ili waweze kusubiri mchakato wa pili wa upigwaji kura

wasanii na wadau wa sekta ya filamu waliojitokeza katika Mkutano wa bodi ya Filamu kutangaza majina ya kazi zilizofanikiwa kuingia kwenye mchujo wa awali katika tuzo za Filamu "Mvuvi na msomi'',"usipite eneo la jeshi","kikao,sitaki ugali",tunaenda kuoa" huku chuchu hansy akifanikiwa kuingiza filamu ''cheupe" na "laura"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...