Na.Khadija Seif,Michuzi TV 

WAZIRI wa nishati, January Makamba amewataka watanzania kutoweka vikwazo katika kutafuta njia pekee ya kuondokana na nishati chafu badala yake watafute njia Mbadala na kuchangia mawazo ya  nini kifanyike ili kurahisisha upatikanaji wa nishati safi na salama ya kupikia  kwa Taifa zima .

Makamba ametoa kauli hiyo  leo Novemba 2 wakati  akiendelea kuongoza mjadala wa  kitaifa wa siku ya pili wa nishati safi ya kupikia ambao unalenga kuweka Sera ,sheria na mifumo mizuri itakayowezesha watanzania kupata nishati safi .

Aidha amefafanua zaidi kuwa ili kupata mafanikio kwa taifa zima ya upatikanaji wa Nishati safi na Salama serikali itahakikisha Sera ,sheria na mifumo madhubuti inawekwa vizuri  huku akiwataka wadau ambao wanafikiri kuanzisha nishati safi mbadala kujitokeza kwani atashirikiana nao katika kutatua changamoto hiyo.

Nae Mbunge wa jimbo la Manonga na Makamu Mwenyekiti Kamati ya kudumu ya Nishati na madini, Seif Khamis Gulamali akishiriki mjadala huo amesema ni kilio cha muda mrefu cha Kamati na wabunge kwa ujumla na wananchi juu ya matumizi mbadala ya Nishati. 

"Ni kilio cha muda mrefu cha Kamati na wabunge Kwa ujumla na wananchi juu ya matumizi mbadala ya Nishati ya mkaa na kuni Kwa sababu tumeona madhara ambayo yanatokea katika jamii zetu.

Aidha,amesema kukatwa kwa misitu si tu inaharibu mazingira na bali pia  inaathiri upatikanaji  wa mvua.

"Mnapokata Miti maana yake kunakuwepo Kwa janga la ukosefu wa mvua na njaa ambayo inawaumiza wananchi wenyewe wananchi" Mh. Seif Khamis Gulamali, Mbunge wa jimbo la Manonga na Makamu Mwenyekiti Kamati ya kudumu ya Nishati na Madini.

Waziri wa Nishati January Makamba akizungumza mara baada ya kukamilika mjadala wa siku ya pili wa nishati safi ya kupikia unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC)Jijini Dar es salaam  ikijumuisha wadau na taasisi mbalimbali 
Makamu Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Kanali  Mstaafu Abdulrahmani Kinana akifatilia kwa kina kitabu cha yaliyomo pamoja na ratiba ya Mjadala wa  Kitaifa wa siku ya pili wa Nishati safi ya kupikia  unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere(JNICC) Jijini Dar es salaam

Mbunge wa Jimbo la Manonga na Makamu Mwenyekiti Kamati ya kudumu ya Nishati na Madini Seif Khamis Gulamali akizungumza kuhusu mjadala wa kitaifa wa siku ya pili wa nishati safi ya kupikia huku akiweka wazi kuwa ni kilio cha muda mrefu kwa namna kamati yake ilikua inafanya mchakato wa kupata nishati safi ambayo haitoathiri chochote ikiwemo sekta ya Afya pamoja na Mazingira. 




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...