Mkutano huo umefanyika leo Novemba 25, 2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Julias Nyerere na kuhudhuriwa na wajumbe wa TATCA, Wajumbe wa Chama cha Waongozaji Ndege Kenya (KATCA), Wajumbe wa Chama cha Waongozaji Ndege Uganda (UGATCA), Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania, wawakilishi wa vyama vingine vya usafiri wa anga Tanzania (TAISOA na TATSEA) pamoja na Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi TUGHE Bi. Jackline Ngoda.

Mkurugenzi wa Udhibiti Uchumi wa TCAA Bw. Daniel Malanga akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 42 wa mwaka wa Chama cha Waongozaji Ndege Tanzania (TATCA). Bw. Malanga alifungua mkutano huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TCAA.
Kaimu Rais wa Chama cha Waongozaji Ndege Tanzania (TATCA) Bw. Limis Makoloela akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 42 wa mwaka wa chama hicho.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Tawi la TCAA (TUGHE) Bi. Jackline Ngoda akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 42 wa mwaka wa Chama cha Waongozaji Ndege Tanzania (TATCA).













Picha ya pamoja 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...