Na Mwandishi Wetu
TIMU ya taifa ya Morocco imeendelea kuchanja mbuga katika Michuano ya Kombe la Dunia, 2022 nchini Qatar baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ngumu ulimwenguni ya Ubelgiji ikiwa ni mchezo wa Kundi F la Michuano hiyo.

Mabao ya Morocco katika mchezo huo yamefungwa na Kiungo Mshambuliaji wa timu hiyo, Abdelhamid Sabiri dakika ya 73’ na bao la pili limefungwa na Mshambuliaji, Zakaria Aboukhlal.

Morocco wakiwa wanakilisha bara la Afrika katika Michuano hiyo, hadi sasa wana alama nne wakiwa wanaongoza Kundi hilo la F, huku wakiwa na alama tatu, Croatia alama moja sawa na Canada wenye alama hiyo moja pekee.

Mchezo wa mzunguko wa mwisho Morocco watacheza dhidi ya Canada huku Ubelgiji watakabiliana na Croatia ili kupata timu mbili zitakazofuzu hatua ya 16 ya Michuano hiyo inayoendelea nchini Qatar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...