Na Mwandishi Wetu
TIMU ya taifa ya Ujerumani imepata alama moja pekee katika michezo miwili ya Kombe la Dunia 2022 inayoendelea nchini Qatar, baada ya kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya taifa ya Hispania kwenye dimba la Al Bayt.

Kwenye mchezo huo Hispania walipata bao lao kupitia kwa Mshambuliaji Alvaro Morata katika dakika ya 62’, huku bao la kusawazisha la Ujerumani likifungwa na Nicolas dakika ya 82’.

Msimamo wa Kundi E, Hispania wanaongoza msimamo wakiwa na alama nne, huku Japan na Costa Rica wote wakiwa na alama tatu, Ujerumani wana alama moja pekee.

Ujerumani, Hispania wamebakisha mchezo mmoja kila mmoja kumaliza mzunguko wa tatu wa Kundi E, Ujerumani watacheza dhidi ya Costa Rica huku, Hispania watacheza na Japan.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...