Na John Walter- Babati


RAIS Samia Suluhu Hassan amezindua barabara za Mitaa za Mji wa Babati kilometa 8.1 na kuahidi kujenga bararaba za lami umbali wa kilometa tano katika Mji huo.

Amezindua barabara hiyo Novemba 212,2022 na kutoa ahadi hiyo mara baada ya kuzindua barabara.

Amesema serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara ili kusaidia wananchi kufanya shughuli zao.

Vile vile alizindua vihenge na maghala ya kuhifadhia mazao ambavyo vimejengwa Mjini Babati ili kulinda usalama wa chakula.

Naye waziri wa kilimo Hussein Bashe amemshukuru Rais kwa kuzindua vihenge hivyo na aliahidi kuwa hadi kufikia mwaka ujao serikali inataka iwe ina uwezo wa kuhifadhi tani 500,000 Nchi nzima.

Akitoa taarifa ya mradi  huo Ofisa mtendaji mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula (NFRA) Milton Lupa amesema kukamilika kwa mradi huo katika eneo la Babati kumeongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kufikia tani 79,000 kwa Kanda ya Arusha ambayo inajumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro  na Manyara.

Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa Babati  wameishukru serikali kwa kujenga vihenge hivyo na kuzindua barabara ambayo imewaondolea vumbi katika mji wa Babati.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...