Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Michael anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kutokana na utata wa kifo cha anayedaiwa kuwa mke wake Primrose Matsambire (39) raia wa Zimbabwe .

Primrose amefariki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi januari 11 alipopelekwa kupatiwa matibabu baada ya kukutwa akiwa anatokwa na damu mdomoni akiwa nyumbani kwake Kiluvya Madukani Wilaya ya Kisarawe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Pius Lutumo alieleza ,aliyegundua marehemu kutokwa damu kwa wingi mdomoni ni msichana wa kazi, baada ya kuona hali hiyo ya marehemu alienda kuomba msaada kwa majirani ambao walifika na kumpeleka katika hospitali ya Tumbi kwa matibabu.

Alisema mume wa marehemu hakuwepo wakati tukio hilo likitokea na kwamba anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano na uchunguzi wa kina wa kifo cha mke wake.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Tumbi huku chanzo cha kifo hicho kikiendelea kuchunguzwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...