Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba amepongeza juhudi zinazofanywa na sekta ya kibenki katika kuimarisha mwelekeo wa ujumuishaji wa fedha nchini.


Akizungumza katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na wanachama wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) jijini Dar es salaam jana, Gavana Tutuba alipongeza safari ya mabadiliko ya kidijitali ambayo benki ya biashara imeanza katika kutoa urahisi na kufikia wigo mpana wa wateja. "Utendaji imara wa benki katika mwaka uliopita ni ushuhuda wa mawazo ya kibunifu yaliyowekwa na benki kuvutia wateja zaidi na kuwapa uzoefu bora. 

Serikali inatambua kazi nzuri ambayo benki hizo zimekuwa zikifanya katika kupanua huduma za kifedha kwa watanzania walio wengi, wakiwamo katika sekta rasmi ya fedha. Naipongeza TBA kwa jitihada zake mbalimbali kwa miaka mingi na nazipongeza benki kwa utendaji wao mzuri wa kifedha. BOT yaahidi mwendelezo wa mashirikiano, " alisema Gavana Mkuu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Mabenki Tanzania (TBA), Theobald Sabi, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya Taifa (NBC), alitoa shukrani kwa niaba ya TBA kwa serikali na Benki Kuu Tanzania (BOT) kwa ushirikiano na jitihada endelevu katika kukuza mazingira mazuri ya kibiashara. "TBA inatambua ushirikiano na msaada kutoka Serikalini na BOT ambao umesababisha sekta kupiga hatua kubwa. 

Kwa mfano, kufikia Desemba 2022, Benki za Tanzania zilipata faida ya zaidi ya sh1.164 trilioni, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia kuzidi ile alama ya faida ya trilioni. Tumeona pia ukuaji mkubwa katika maeneo mengine, kama vile huduma za kibenki kupitia mawakala, kidijitali, mikopo kwa sekta binafsi, na miongozo ya biashara yenye kujenga ambayo imetufanya kustawi. Tunashukuru sana," alisema Sabi.

Aidha naye, Mkurugenzi Mtendaji wa TBA, Tuse Joune alisema kuwa TBA kwa sasa inatekeleza Mkakati wa Miaka Mitano (2023-2027) ambao utazinduliwa hivi karibuni kwa umma. "Nina furaha kutangaza kwamba mpango wetu wa miaka mitano (2023-2027) sasa uko tayari kwa uzinduzi, na hivi karibuni tutaupeleka kwa umma," alisema.

Mbali na kumkaribisha Gavana Tutuba, TBA pia ilitumia hafla hiyo kumuaga Gavana wa Benki Kuu Tanzania(BOT) anayemaliza muda wake, Prof. Florence Luoga, ambaye amestaafu.

Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BOT),Emmanuel Tutuba Akimkabidhi zawadi Gavana wa Benki Kuu anayemaliza muda wake, Prof. Florence Luoga, ambaye amestaafa katika hafla iliyoandaliwa  na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) mwishoni wa wiki iliyopita . Anayeshuhudia kulia ni Mwenyekiti wa  Chama cha Mabenki Tanzani (TBA), Theobald Sabi,na kushoto Ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBA Bi. Tuse M. Joune .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...