Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) imeungana na wadau wa elimu wa mkoani Tanga, kupambana na unywaji pombe kwa watu wenye umri mdogo ili kudhibiti tabia ya unywaji pombe miongoni mwa wanafunzi wa shule.

SBL imeshirikiana na Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa Jiji la Tanga, Maurus Ndunguru na Afisa Maendeleo wa Jiji la Tanga na Mratibu Mashirika ya Kijamii Naetwa Kilango, kusambaza elimu ya kuepuka matumizi ya pombe kwa wanafunzi katika halfa maalum iliyofanyika katika shule ya sekondari Nguvumali.

Kampeni hiyo iliyopewa jina la SMASHED, ni kampeni ya kupambana na unywaji wa pombe ya SBL, inayotumia michezo ya kuigiza ya jukwaani inayowapa uezofu wa kipekee na kusisimua. Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zenye kundi la watu wenye umri mdogo wa wanaotumia pombe.

Utafiti uliofanywa mwaka 2019 katika mikoa ya Mwanza na Kilimanjaro ulibaini kuwepo kwa mwenendo wa matumizi ya pombe miongoni mwa wanafunzi wa shule za sekondari wenye umri wa miaka 15 na zaidi ni kutoka asilimia 12.9 miongoni mwa wasichana mkoani Mwanza hadi asilimia 63.9 miongoni mwa wavulana mkoani Kilimanjaro.

SMASHED hufanyika mashuleni na huelimisha wanafunzi wa sekondari kuhusu madhara ya matumizi ya pombe katika umri mdogo, kwa kuwashauri kujiepusha na matumizi ya pombe kabla ya kukomaa.

Programu hii inachanganya matumizi ya maonyesho ya maigizo na ushiriki wa wanafunzi katika mazingira ya motisha ya kujifunza ili kuwapa ukweli, ujuzi na ujasiri wa kufanya uchaguzi wa kuwajibika na kuendeleza mitazamo ya uwajibikaji katika masuala yanayohusiana na afya.

Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa Jiji la Tanga, Maurus Ndunguru, alipongeza SBL kwa kampeni ya SMASHED na kutoa mapendekezo zaidi.
“Kampeni hii itasaidia sana vijana wetu wa shule, hasa katika shule hizi tano mlizozifikia, maana wanafunzi wamekuwa wakipata changamoto za ulevi. Nashauri pia, kampeni hii iweze pita katika shule zote mkoani Tanga” Alisema Ndunguru.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mahusiano ya Umma wa SBL alisema "SMASHED inatoamafunzo muhimu juu ya athari mbaya za unywaji pombe katika umri mdogo kwa vijana na jamii,kwa makusudi mazima ya kulinda ndoto na ustawi wa vijana, ili kuhakikisha wanafanikiwa katika
jitihada zao".

Wanyancha alisema mpango huo umetekelezwa nchi nzima tokea Oktoba 2022 kwa awamu,kuanzia Dar es Salaam na kuhamia mkoani Tanga. Zaidi ya wanafunzi 15,000 wamefikiwa nampango huo katika mikoa hiyo miwili.

Afisa Maendeleo wa Jiji la Tanga na Mratibu Mashirika ya Kijamii Naetwa Kilango
amefurahishwa na mbinu za kibunifu za utoaji elimu kwa vijana na kuwaomba wadau wenginekubuni miradi ya kulinda ndoto za wanafunzi.

"Ahsanteni Serengeti Breweries kwa ushirikiano wenu katika kuwaasa vijana hawa na kuwapambinu za kulinda kesho yao. Kwa kweli vitendo vya matumizi ya pombe katika umri mdogo ni lazima vipigwe vita na SMASHED ni jukwaa muhimu sana", alisema Kilango.

Kwa upande mwingine, Ocheck Msuva mwanzilishi wa asasi ya kiraia ya vijana, Bridge for Change inayotumia sanaa ya maigizo ya jukwaani kufikisha ujumbe, amesema SBL inawapa vijana nafasi ya kupanga kesho yao wakiwa na maarifa ya kutosha kufanya maamuzi makini.

“Ikiwa vijana watakuwa na uelewa, maarifa na elimu juu ya madhara ya urahibu wa vilevi ni stahiki kabisa watakuwa na nafasi ya kufanya maamuzi sahihi ambayo ni kiini cha kuelekea katika njia ya mafanikio.” Alisema Ocheck.
Kampeni hiyo ya SMASHED imekelezwa ndani ya shule tano za sekondari jijini Tanga, nazo ni:
Nguvumali, Kihere, Toledo, Masechu na Mnyanjari sekondari.

Waigizaji wa Maigizo ya Jukwaani, Mudrik Abdy (aliyelala), Halua Mkilindi (kulia) na Davidi Sayi (Kusho-mwisho) wakionyesha madhara ya ulevi kupitia igizo maalum, ikiwa ni sehemu ya somo katika kampeni ya kupinga unywaji pombe katika umri mdogo ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ijulikanayo kama “SMASHED”. Kampeni hiyo imefanyika katika shule tano jijini Tanga, ikiwemo Shule ya Sekondari Nguvumali, mapema leo.

Waigizaji wa Maigizo ya Jukwaani, Halua Mkilindi (kulia) na Davidi Sayi (Kusho) wakionyesha madhara ya ulevi kupitia igizo maalum, ikiwa ni sehemu ya somo katika kampeni ya kupinga unywaji pombe katika umri mdogo ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ijulikanayo kama “SMASHED”. Kampeni hiyo imefanyika katika shule tano jijini Tanga, ikiwemo Shule ya Sekondari Nguvumali, mkoani Tanga, mapema leo.


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nguvumali wakifurahia igizo la ucheshi la kuasa wanafunzi na matumizi ya pombe, katika kampeni ya SMASHED ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), iliyofanyika katika shule hiyo, mkoani Tanga, mapema leo.


Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa jiji la Tanga Maurus Ndunguru (Kulia) akiongea na wanafunzi wakatika wa hafla maalum ya utoaji elimu ya unywaji pombe kwa umri mdogo ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) SMASHED. Pembeni ni Ocheck Msuva  (Kushoto) Mkurugenzi wa Taasisi ya Bridge for Change inayotumia michezo ya kuigiza ya jukwaani katika kampeni ya SMASHED. Tukio hilo limefanyika katika shule ya sekondari ya Nguvumali, iliyopo Tanga,  mapema leo.


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nguvumali, wakiangalia igizo la jukwaani la kuwaasa dhidi ya matumizi ya pombe katika umri mdogo, lililofanyika mapema leo jijini Tanga.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...