Benki ya Exim Tanzania imekutana na wateja wake wadogo na wakubwa wa jijini Arusha ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya, sambamba na kuwaelimisha wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo huku Mkuu wa Mkoa huo Bw John Mongella akiipongeza benki hiyo kwa mchango wake katika kuchochea mabadiliko ya kiuchumi ya mkoa kupitia huduma zake kwa wadau mbalimbali wakiwemo wawekezaji kwenye sekta ya utalii, biashara na viwanda.


Akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo mwishoni mwa wiki mahususu kwa wateja hao, RC Mongella alisema mchango wa benki hiyo yenye matawi manne mkoani humo unaonekana zaidi kupitia huduma zake zinazoendana na mahitaji halisi ya wateja wake mkoani humo.

“Natoa pongezi hizi nikiwa na uhakika kwasababu mimi binafsi pia ni mteja wa muda mrefu wa benki ya Exim na sijawahi kujilaumu kwenye hilo. Katika kipindi cha miaka 20 ambayo mpo hapa Arusha mmekuwa karibu zaidi na wakazi wa mkoa huu mkitoa suluhisho la huduma za kifedha kulingana na mahitaji na aina uwekezaji wanaoufanya. Wingi wa matawi yenu mkoani Arusha unathibitisha hilo hongereni sana,’’ alisema.

Kwa mujibu wa Bw Mongella kwa sasa mkoa huo upo kwenye kasi kubwa ya mabadiliko ya kiuchumi yanayochagizwa na ukuaji wa sekta ya utalii, biashara, kilimo na viwanda hivyo maboresho ya kihuduma yanayofanywa na taasisi za kifedha ikiwemo benki ya Exim yatakuwa na mchango kwa wadau wengi waliopo kwenye sekta hizo.

“Wito wangu kwenu benki ya Exim na taasisi nyingine za kifedha muendelee kukutana na wateja wenu mara kwa mara muwasikilize kwa kuwa mrejesho mtakao upata utawasaidia kubuni huduma zenye majawabu kwao.’’ Alisema RC Mongella huku akionesha kuvutiwa na huduma mpya ya Supa woman inayotolewa na benki hiyo mahususi kwa wanawake.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Bw Jaffari Matundu alisema benki hiyo imedhamiria kufanya maboresho makubwa katika utoaji huduma kwa wateja wake kwa kutilia mkazo katika maeneo muhimu, ambayo ni uboreshaji wa mifumo na taratibu za utoaji huduma, ili ziendane na mahitaji halisi ya wateja na soko.

“Zaidi, kupitia mkakati huu mpya tumejipanga kuongeza weledi zaidi na umahiri wa wafanyakazi wetu, kuwekeza kwenye teknolojia ya kisasa pamoja na kukuza biashara katika nyanja zote ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Rais Samia Suluhu.’’ Alisema Bw Matundu aliembatana na maofisa wengine waandamizi kwenye hafla hiyo.

Alisema imani kubwa inayooneshwa na wateja hao kwa benki hiyo imekuwa sababu kwao kuwa nao bega kwa bega huku akitolea mfano katika kipindi cha changamoto za kibiashara zilizowakumba wateja wa benki hiyo hususani wale waliopo kwenye mnyororo wa biashara ya utalii kutokana na mdororo wa kibiashara uliotokana na janga la COVID 19.

“Benki ya Exim tulikuwa pamoja nao na tulichukua hatua za makusudi kwa kuhakikisha tunatoa likizo ya urejeshaji wa madeni hadi pale hali ya kiuchumi ilipoanza kurejea katika hali ya kawaida…huu ndio urafiki wa kweli.’’ Alisisitiza.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi na bishara za kati wa Benki ya Exim Tanzania, Andrew Lyimo alisema utambulisho wa huduma mpya za benki hiyo ikiwemo akaunti ya wajasiriamali, akaunti ya Supa Woman, huduma ya benki isiyo na mipaka (borderless banking) mahususi kwa wafanyabiashara wa Tanzania na Comoro na huduma nyingine za kisasa kwa ajili ya malipo umekuja kuongeza nguvu kwenye huduma kongwe zinazotolewa na benki mahususi kwa wateja wa mkoa huo ikiwemo huduma ya kadi ya Exim TANAPA.

“Lengo ni kurahisisha huduma zaidi na kuondoa usumbufu kwa wateja wetu na ndio sababu tunawekeza zaidi kwenye huduma za wakala ambapo hadi kufikia sasa tuna mawakala zaidi ya 120 nchi nzima na tunaendelea kufanya uwekezaji zaidi kwenye huduma za kielektroniki,’’ alisema Bw Lyimo huku akisisitiza kuwa benki hiyo inatoa kipaumbele kwenye huduma za mikopo kwa wateja wa aina mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa Arusha Bw John Mongella  akizungumza na wageni waalikwa  wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja wa Benki ya Exim Tanzania  mkoani humo iliyofanyika mwishoni mwa wiki ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.


Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Bw Jaffari Matundu akizungumza na wageni waalikwa  wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja wa benki hiyo mkoan wa Arusha iliyofanyika mwishoni mwa wiki ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.


Mkuu wa Mkoa Arusha Bw John Mongella (Kulia) akibadilishana mawazo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Bw Jaffari Matundu (kushoto) wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja wa benki hiyo mkoani humo iliyofanyika mwishoni mwa wiki ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.


Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi na bishara za kati wa Benki ya Exim Tanzania, Andrew Lyimo (alievaa koti la bluu) akibadilishana mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo mkoa wa Arusha wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja hao  iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha  ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.


Mkuu wa Matawi wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Agnes Kaganda (kushoto) akiwakaribisha baadhi ya wateja wa benki hiyo mkoa wa Arusha wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja hao  iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha  ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.



Baadhi ya wageni waalikwa ambao ni  wateja wa benki ya Exim Mkoa wa Arusha wakiwa kwenye hafla hiyo.


Mkuu wa Mkoa Arusha Bw John Mongella  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa benki ya Exim Tanzania pamoja na baadhi ya wateja wa benki hiyo mkoani humo wakati wa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wateja hao iliyofanyika mwishoni mwa wiki ikilenga kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika mkoa huo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...