Na. WAF - Dodoma

Serikali imedhamiria kuendelea kushirikiana na wadau katika sekta zote ili kudhibiti na kuutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) ifikapo mwaka 2030.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi kwenye kikao na Makatibu Wakuu wa Wizara kilichofanyika katika ofisi za Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

“Ili kudhibiti ugonjwa huu wa Kifua Kikuu ni muhimu kushirikiana na wadau wengi kama sekta ya afya, wadau sekta ya elimu, sekta ya usafirishaji na sekta nyingine mbalimbali.” amesema Dkt. Yonazi

Kwa upande wake Mtaalamu Mshauri kutoka Stop Tb Partnership (STP) Bw. Oscar Mukasa wakati akiwasilisha taarifa ya mpango kazi wa kudhibiti Kifua Kikuu amesema watu wenye hatari zaidi ya kupata Kifua Kikuu ni pamoja na watu wanaoishi kwenye makazi duni, Watoto, Wavuvi na Wanaoishi Bweni.

Pia, amesema Watu wenye VVU, watu wenye Utapiamlo, wachimbaji madini, wanaoishi na mgonjwa wa Kifua Kikuu, watoa huduma za afya na wanaotumia madawa ya kulevya kwa kujidunga sindano.

Mwisho, Bw. Mukasa amewashauri wanaoishi katika mazingira hayo kuchukua tadhari za kujikinga na ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...